BREAKING
  • FANGASI UKENI

    Pata suluhisho la tatizo la fangasi ukeni pamoja na ushauri utakaokufanya uwe salama daima

  • TIBA YA NGUVU ZA KIUME

    Okoa nyumba yako kwa kupata dawa itakayo ongeza nguvu zako za kiume na kudumisha unyumba daima

  • SULUHISHO LA U.T.I

    Je hauna ufahamu wowote kuhusu U.T.I ?Je Unakabiliwa na tatizo la U.T.I?Wasiliana nami nikujuze zaidi huenda una tatizo la U.T.I lakini haujijui,na kama unalo basi tiba yake ipo

  • TIBA YA VIDONDA VYA TUMBO

    Je Umesumbuliwa na vidonda vya tumbo kwa muda mrefu pasina kupata suluhisho,wasiliana nami nikupatie dawa itakayoondoa tatizo lako kabisa

BannerFans.com

Jumatano, 11 Januari 2017

SULUHISHO LA TATIZO LA WANAWAKE KUOTA NDEVU NA MANYOYA(HIRSUTISM)

FAHAMU TATIZO LA WANAWAKE KUOTA NDEVU NA MANYOYA(HIRSUTISM}

Asalaam alaykum warhmatullah wabarakatul, ni matumaini yangu unaendelea vyema mpendwa msomaji
Naam ni jambo la kumshukuru Allah kuiona siku mpya kila siku haijalishi unaumwa ama una magumu unapitia USITAMANI KUFA KWANI KILA TATIZO LINA SULUHISHO LAKE hivyo mshukuru Allah kwa kila kitu katika maisha yako
Ama baada ya salam Leo ni vyema tukapata darasa kuhusiana na kichwa cha habari hapo juu

HIRSUTISM NI NINI?

Ni ugonjwa ambao wanawake hupatwa na mabadiliko ya  kuotwa manyoya sehemu ambazo kikawaida wao hua hawaoti manyoya maeneo hayo
mfano ndevu kidevuni, manyoya kifuani, usoni, na mgongoni wakati mwingine manyoya magumu kama ya kiume miguuni na mikononi

Kikawaida wingi wa manyoya mwilini mwa binadamu hutegemea sana vimelea vya ukoo husika, kitaalamu kama genetics make up lakini mwanamke anapokua na manyoya mengi kama ya mwanaume hasa ndevu kuna mambo makuu mawili kwamba anaumwa au ukoo wake uko hivyo japokua waathirika wengi wa shida hii ni wagonjwa

DALILI ZA HIRSUTISM

Kawaida gonjwa wa hirsutism huwa na dalili za kua na manyoya mengi kama nilivyotaja hapo juu lakini pia mgonjwa huweza kua na sauti nzito kama kama mwanaume, kuota kipara, kinembe kua kikubwa, chunusi na kupungua ukubwa wa matiti

CHANZO/VISABABISHI VYA TATIZO

Kawaida mwanamke akibaleghe huanza kutengeneza homoni za kiume na za kike ndio maana manyoya huota kwapani na maeneo ya uke hivyo homoni za kiume zikiwa nyingi kitaalamu kama adrogens mwanamke hupata hali hii ya kuota manyoya sehemu ambazo hazihusiki kama nilivyotaja hapo juu
 lakini pamoja na hali hii ugonjwa huu una vyanzo vingine kama vifuatavyo.

POLYCYSTIC OVARY SYNDROME: huu ni ugonjwa unaotokana na kutokuwa na uwiano sawa wa homoni za mwanamke kitaalamu kama homornal imbalance hivyo mwanamke hupata mzunguko wa damu ambao sio wa kawaida, kua mgumba,  kunenepa na kupata uvimbe kadhaa kwenye ovari za kutengeneza mayai yake.

MATUMIZI YA DAWA NA VIPODOZI VYENYE KEMIKALI
hii huenda ndio ikawa chanzo kikuu cha wanawake wengi kuota ndevu na manyoya  kwa tabia ya kutumia dawa fulani bila maelekezo ya daktari pia siku hizi kuna maduka ya urembo yanauza dawa hizi na kuzigeuza dawa za urembo wakati ni hatari  sana kiafya kwa watumiaji. kuna dawa kitaalamu zinaitwa steroids huingilia mfumo wa kiungo kinachohusika na utengenezaji wa homoni{ adrenal gland] hivyo zikitumika kwa muda mrefu huleta manyoya ambayo sio ya kawaida kwa wanawake mfano predinisolone vidonge na cream, sonaderm, candiderm,gentaline c, na dawa zingine zote zenye mchanganyiko huu kwani zipo nyingi ila mchanganyiko ni uleule ila majina tofauti ya viwanda. Dawa hizi hutakiwa zitumike kwa angalau wiki moja tu kutibu ugonjwa wa ngozi lakini wengine wamezigeuza kama mafuta ya kujipaka hivyo kama na wewe unapaka hizo aina za dawa ujue ndevu ziko njiani.

UVIMBE WA KANSA
kansa za kiungo hichi kilichopo juu ya figo[adrenal gland] huongeza wingi wa homoni hizi kwenye mfumo wa binadamu na kuleta ndevu na manyoya magumu ya mwili.

CONGENITAL ADRENAL HYPERPLASIA:
huu ni ugonjwa wa adrenal gland ambao mtu huzaliwa nao na kuanza kutoa homoni nyingi za uzazi na matokeo yake mtu huota ndevu na manyoya mengi mwilini..

CUSHING SYNDROME:
hali hii hutokea baada ya mgonjwa kupata matibabu ya dawa zenye homoni ya  cortisol mwilini mwake kwa muda mrefu. Mfano matumizi ya dawa ya prednisolone vidonge  kwa wagonjwa wa allergy na asthma.

Wakati mwingine ugonjwa huu hutokea bila sababu yeyote hasa kwa jamii za kiarabu na kihindi

VIPIMO:

Mgonjwa anashauriwa kupima kipimo kuangalia wingi wa homoni mwilini wake hasa testosterone kama zitakua zipo juu Au kupiga picha ya ultrasound ya ovary kuangalia kama kuna tatizo lolote au kupima kuangalia uvimbe wa adrenal gland  mara nyingi ni moja ya vyanzo vikuu.

MATIBABU

Mara nyingi kutafuta chanzo cha ugonjwa na kutibu ni moja ya matibabu bora zaidi lakini pale ambapo  chanzo hakionekani dawa zifuatazo zinaweza kutumika kutatua tatizo hilo

SOY CAPSULES 500MG
 hivi ni vidonge vilivyotengenezwa kiasili ambavyo husaidia sana kupanga homoni za uzazi katika hali ya kawaida na kubalance homoni,kuondoa ukavu ukeni na kuleta hamu ya tendo la ndoa pia ni msaada mkubwa kwa wenye matatizo ya uzazi

SPIRONOLACTONE;
hizi pia hutumika kuzuia homoni za kusababisha manyoya lakini ukitumia dawa hizi lazima utumie uzazi wa mpango kwani zinasababisha madhara makubwa sana kwa mtoto ikitokea  ukibeba  mimba wakati unaendelea na dozi hiyo.

DAWA YA KUPAKA YA EFLORNIRITHINE;
 Dawa ya  Eflornithine  kitaalamu hutumika kupakwa maeneo yalioathirika na nywele nyingi kuzuia kasi ya kukua lakini hazitoi manyoya yaliyopo.

LASERS THERAPY
 hii ni miale ya mwanga ambayo inapita ndani ya ngozi kuzuia vyanzo vya ngozi{hair follicles} kuota tena mara nyingi hufanya kazi vizuri lakini gharama yake ni kubwa mno na huenda haipatikani kirahisi.



VEET CREAM :
 hii ni cream inayopatikana madukani kwa bei za kawaida ukipaka inanyoa manyoya yote japokua baada ya muda yataota tena lakini inasaidia sana hasa ukipaka mara mara kwa mara au mara moja au mbili kwa wiki.

 ELECTROLYSIS:
hii inahusisha kuweka sindano ndogo  maalumu kwa kila shimo la unywele na kuharibu chanzo chake ni moja ya matibabu mazuri ila ina maumivu makali sana na dawa za nganzi za kupakwa hutumika kupunguza maumivu hayo.

NOTED; kama wewe ni mwanamke una ndevu au manyoya ambayo sio ya kawaida na huenda mwanzoni hayakuepo angalia kwa makini vipodozi vyako huenda ndio vinasababisha lakini pia nenda hospitali ukachunguzwe wingi wa homoni na upigwe picha ya viungo vya uzazi kama viko salama. ushauri wa bure ni kwamba serikali imekua ikipiga marufuku baadhi ya vipodozi na kuvichoma moto lakini watu wanahisi wanaonewa na kuvitafuta kwa magendo, ukiona kitu kimepigwa marufuku achana

Mpendwa msomaji nashukuru Kwa kuchukua muda wako kufatilia makala zangu za afya nasema ASANTE NA MUNGU AKULIPE KHERY PIA IKIWA UNA MAONI AU USHAURI NIANDIKIE UJUMBE  KUPITIA KATIKA EMAIL AU NAMBA ZANGU HAPO CHINI

KUSOMA ZAIDI MAKALA MBALIMBALI  ZA AFYA TEMBELEA
 NAYTHAMHEALTHCARE.BLOGSPOT.COM

 ~Makala hii imeandaliwa na Dr Naytham Salum
E-mail nsalum998@gmail.com
+255623026602/+255746465095

PLZ USISAHAU KUSHARE, KUKOMENT, KULIKE NA WATAG RAFIKI ZAKO WAJIFUNZE

Jumapili, 8 Januari 2017

FAHAMU SULUHISHO SAHIHI LA PUMU

FAHAMU UGONJWA WA PUMU NA TIBA YAKE

Asalaam alaykum warhmatullah wabarakatul, ni matumaini yangu wote tuwazima alhamdulillah kwa nafasi ya kukutana tena hapa kupata somo la afya kuhusu ugonjwa wa pumu ambao umekuwa ukiwatesa watu sana
Naam

Ugonjwa wa pumu ni ugonjwa ambao huathiri sehemu ya kupitisha hewa kwenda kwenye mapafu ya binadamu zinazojulikana kitaalamu kama bronchioles. Mtu mwenye pumu huwa na mcharuko mwili sugu (chronic Inflammation) kwenye mirija yake ya

kupitishia hewa (bronchioles tubes)hali ambayo husababisha kuvimba kwa kuta za mirija hii, kujaa kwa ute mzito (mucus) na kupungua kwa njia ya kupitishia hewa, hali ambayo humfanya muathirika kushindwa kuvuta na kutoa hewa

nje na hivyo kupumua kwa shida sana. Hali hii inaweza kudumu kwa muda mfupi au mrefu kiasi cha kuhitaji tiba ili kumuwezesha mgonjwa kupata nafuu. Kutokana na kuwepo kwa msuguano na uzuiaji wa kupitisha hewa wakati wa kupumua hwa nje, pumu hujulikana pia kama obstructive lung disease . Mtu aliye na pumu, huwa nayo kipindi chote cha maisha yake.

MAKUNDI YA PUMU

Pumu inaweza kugawanywa katika makundi mawili;
Pumu ya ghafla (Acute asthma): Wagonjwa wanaopatwa na kundi hili la pumu huwa na hali ya kawaida katika njia zao za hewa isiyobadilika kati ya shambulizi moja na jingine.Pumu sugu (Chronic Asthma): Kundi hili la pumu huwa na tabia ya kuwa na njia nyembamba za kupitisha hewa na kadiri jinsi mgonjwa anavyoendelea kupata matukio zaidi ya pumu, njia za hewa huzidi kuwa nyembamba zaidi.

AINA ZA UGONJWA WA PUMU

Bila kujalisha mgonjwa anaingia katika kundi gani, ugonjwa wa pumu unaweza kugawanywa katika aina kuu nne, ambazo ni 1.Pumu inayobadilika (brittle asthma):Kulingana na tabia ya kujirudia rudia kwa matukio ta ugonjwa huu na madhara yake kwa mgonjwa, aina hii ya pumu inaweza kugawanywa zaidi katika aina nyingine mbili, ambazo ni
Aina ya kwanza ya pumu inayobadilika (type 1 brittle asthma) ni pumu yenye tabia ya kuwa na matukio na mashambulizi ya kubadilika kila mara japokuwa mgonjwa anaweza kuwa anapata matibabu kadhaa.Aina ya pili ya pumu inayobadilika (type 2 brittle asthma) ni pumu ambayo mgonjwa anatokea kupata shambulizi la ghafla(asthmatic attack) wakati hapo awali ugonjwa wake uliweza kuthibitiwa kwa matibabu.2.Pumu hatari isiyobadilika (status asthmaticus): Hii ni aina ya pumu iliyo hatari zaidi kwa mgonjwa. Pamoja na

matumizi ya dawa kadhaa,zikiwemo vitanua njia za hewa(bronchodilators) na vipoza mcharuko mwili (steroids), mgonjwa wa aina hii ya pumu anaweza asipate nafuu ya haraka, na anaweza kupoteza maisha. 3.Pumu

inayosababishwa na mazoezi(Exercise Induced Asthma): Hali hii husababishwa na ufanyaji wa kupitiliza wa mazoezi ya viungo. Kwa kawaida wakati wa kufanya mazoezi mtu hupumua kwa kutumia pua na kupitia mdomoni. Hata hivyo wakati

mwingine hutokea hewa aivutayo huingia ndani ikiwa haijapozwa vya kutosha puani na hivyo kusababisha ongezeko la mtiririko wa damu katika mishipa inayosambaza damu katika mirija ya kupitisha hewa. Hali hii husababisha kuvimba

kwa kuta za mirija hiyo na muhusika kupata shambulizi la pumu. Aina hii ya pumu yaweza kudhibitiwa na dawa. Inashauriwa sana kwa watu wenye matatizo kama haya kupasha moto misuli kwa mazoezi mepesi (warming up)kabla

ya kuanza mazoezi mazito na ya muda mrefu. 4.Pumu inayosababishwa na aina ya kazi afanyayo muhusika (Occupational Induced Asthma): Wakati fulani, mazingira ya kazi yanaweza kusababisha kutokea kwa pumu hata kwa baadhi ya wafanyakazi wasio na tatizo hili. Mara nyingi aina hii huweza kuwatokea watu wanaofanya kazi kwenye viwanda vya kutengeneza matairi, vigae, rangi, kemikali mbalimbali, mbolea, chuma, unga na mbao.

VISABABISHI VYA PUMU

Kuna mambo kadhaa yanayoweza kusababisha kutokea kwa pumu au yanayohusishwa na shambulizi lake. Mambo hayo ni pamoja na
Matatizo ya kinasaba: Matatizo ya kinasaba yamehusishwa na kutokea kwa karibu asilimia 90 ya ugonjwa wa pumu hususani kipindi cha utoto.Uvutaji wa sigara au tumbaku kipindi cha ujauzito pia unahusishwa na kusababisha pumu kwa mtoto atakayezaliwa.Maendeleo ya kiuchumi: Ugonjwa wa pumu umeonekana sana kwenye nchi zilizoendelea kiuchumi ikilinganishwa na nchi zenye maendeleo na hali duni ya kiuchumi.Magonjwa ya mapafu kamabronchitisVyanzo vya mzio(allergens)kama vile vumbi, vinyesi vya wanyama na baadhi ya vyakula.Uchafuzi wa mazingira kama moshi na baadhi ya harufu kali.Baadhi ya kemikali kwenye maeneo ya kazi hasa kwenye viwanda kama vya rangi, chuma, sementi na vigae.Baadhi ya wagonjwa wanaotumia dawa za kushusha shinikizo la damu zilizo katika jamii ya beta-blockers kama vile propanololwapo katika hatari ya kupata shambulio la ugonjwa wa pumu.Magonjwa kwenye mfumo wa kupumua yasabishwayo na baadhi ya virusi na bakteria kama vile rhinovirus, Chlamydia pneumonia auBordetella pertusis.Matumizi ya mapema sana ya baadhi ya dawa hasa antibiotiki kwa watoto yanaweza kubadilisha mfumo wa kinga ya mwili dhidi ya magonjwa na hivyo kumfanya mtoto kuwa katika hatari ya kupata pumu.Ongezeko la msongo wa mawazo huweza kusababisha pumu na matatizo katika mfumo wa upumuajiUpasuaji wakati wa kujifungua (caesarian section):Tafiti kadhaa zimeonesha kuwa kujifungua kwa njia ya upasuaji huongeza uwezekano wa kupata pumu kwa vile njia hiyo yaweza kuathiri mfumo wa kinga ya mwili dhidi ya maradhi.Vihatarishi vya ugonjwa wa pumu

Uwezekano wa kupata ugonjwa wa pumu huongezeka iwapo mtu
Atakuwa na magonjwa ya mzio kama vile magonjwa ya ngozi (eczema) au homa isababishwayo na aina fulani ya vumbi (hay fever)Atavuta chavu (pollen) kutoka kwenye maua au mitiAtajihusisha na uvutaji sigaraAna historia ya ugonjwa wa pumu au mzio kwenye familiaUtumiaji wa dawa aina yaaspirinAna msongo wa mawazoAna uambukizi wa magonjwa ya virusi kamarhinovirusMazoeziAnaishi sehemu zenye baridiAna matatizo katika njia yake ya chakula (Gastroesophageal reflux disease au GERD)

DALILI ZA PUMU
Dalili za ugonjwa wa pumu ni pamoja na
Kuishiwa na pumzi na kupumua kwa shida (shortness of breath)Kutoa sauti kama mtu anayepiga miluzi wakati wa kupumua (wheezing)Kukohoa sana (chronic cough)hasa nyakati za usiku au asubuhi. Aidha kikohozi huambatana na kutoa makohozi mazito, yasiyo na rangi au yenye rangi ya njano.Kubana kwa kifua.Kwa mtu aliyepata shambulizi kubwa la pumu (severe asthmatic attack) anaweza kushindwa kuzungumza na pia kuwa na hali kama ya kuchanganyikiwa.Vipimo na Uchunguzi

Pamoja na daktari kutaka kufahamu historia ya mgonjwa, anaweza pia kuamua kufanya vipimo vifuatavyo ambavyo vitamsaidia kufahamu chanzo na madhara ya ugonjwa wa pumu kwa muathirika.
Kipimo cha damu (complete blood count) msisitizo ukiwa kwenye wingi wa seli za damu aina ya eosinophils ambazo uhusika na kuwepo kwa shambulio la mzio.Kipimo cha kuchunguza uwezo wa mgonjwa kutoa hewa nje mara baada ya kuivuta (spirometery). Aina hii ya uchunguzi hufanyika kabla ya mgonjwa kupewa dawa kwa kutumia nebulizer.Kipimo cha kuchunguza kiwango cha hewa ya oksijeni kilichopo kwenye damu ya mgonjwa (oximetry).Kipimo cha kuchunguza uwezo wa mgonjwa kupumua hewa nje wakati wa shambulizi la pumu (Peak flow meter).X-ray ya kifua kwa ajili ya kutofautisha pumu na magonjwa mengine yenye dalili za kufanana kama vile ugonjwa wa moyo (congestive heart failure), magonjwa sugu ya kuziba kwa njia za hewa (COPD kama vile chronic bronchitis na emphysema) na magonjwa mengine ya kuzaliwa kama vile cystic fibrosis.Kipimo cha mzio cha ngozi(skin allergy test) kwa ajili ya kutambua aina ya mzio inayomsababishia mgonjwa shambulizi la pumu.

MATIBABU YA PUMU
Kwa ujumla matibabu ya pumu hujumuisha kuepuka visababishi vya ugonjwa huu na matumizi ya madawa kwa walio na hali mbaya. Aidha, kwa wanaopata ugonjwa huu kwa sababu ya msongo wa mawazo hupewa ushauri nasaha kwa ajili ya

kusaidia kutatua matatizo yanayowakabili. Vilevile inashauriwa kwa wenye tatizo hili, kuwa na dawa karibu muda wote kwa ajili ya matumizi pindi shambulizi litakapotokea. Pia inashauriwa sana kuepuka mazingira na hali za baridi ambazo

huweza kuchochea kutokea kwa shambulio la ugonjwa huu. Matibabu ya kutumia dawa hujumuisha matumizi ya dawa za kusaidia kupunguza na kuondoa makohozi (expectorants), dawa zinazosaidia kutanua mirija ya hewa(bronchodilators), dawa za kuondoa mcharuko mwili kama vile cortisone ya drip (hasa wakati wa dharura) au nebulizer, na dawa za kuzuia

mzio (antihistamine drugs). Hata hivyo, kuna matibabu ya ziada kulingana na hali ya mgonjwa pamoja na kundi na aina ya pumu inayomuathiri mgonjwa. Kwa wagonjwa wenye pumu ya ghafla na wenye hali mbaya (acute asthma)matibabu hujumuisha matumizi ya dawa za kutanua mirija ya hewa(bronchodilators) pamoja na kuongezewa hewa ya

oksijeni, dawa za kutuliza mcharuko mwili (steroids) pamoja na dawa za kutuliza kukakamaa kwa misuli ya mwili (intravenous muscle relaxants). Aidha kwa vile mara nyingi shambulizi hili laweza kuwa la hatari sana, mgonjwa hulazwa

hospitali na huongezewa hewa ya oksijeni, na kwa wagonjwa wasioweza kupumua kabisa, husaidiwa kufanya hivyo kwa kutumia mashine maalum iitwayo(mechanical ventilator). Kwa wagonjwa wenye pumu sugu, jambo la muhimu ni

kuepuka visababishi vya pumu na kuendelea na matumizi ya dawa zinazosaidia katika kutanua mirija ya hewa. Kwa wagonjwa wanaopata mashambulzi ya mara kwa mara wanaweza kushauriwa na daktari kutumia dawa kadhaa zikiwemo zile zinazopunguza mcharuko mwili(mast cell inhibitors, inhaled steroids au oral steroids), pamoja na dawa za

kutuliza kukakamaa kwa misuli ya mwili (muscle relaxants). Aidha ni vema pia kutibiwa na kuthibiti kutokea kwa magonjwa yote yahusuyo mfumo wa hewa. Matumizi ya chanjo ya magonjwa kama influenza na pneumococcal pneumonia nayo husaidia sana katika uthibiti wa kutokea kwa pumu. Ni vema pia kuepuka matumizi ya dawa za jamii ya beta-blockers kwa wagonjwa wenye shinikizo la damu na ambao pia wana pumu.

DAWA MBALIMBALI UNAZOWEZA TUMIA KUTIBU PUMU

KITUNGUU THOMU

Kitunguu swaumu

Chukua punje 5 hadi 6, menya na ukate vipande vidogo vidogo lakini siyo vidogo sana na uchemshe kwenye moto na maji kikombe kimoja (robo lita), ongeza kijiko kikubwa kimoja chaasali mbichi ndani yake na uache kwenye moto kama dakika 5. Ipua na unywe kwa pamoja kutwa mara 2 hadi utakapopona.



TANGAWIZI

Tangawizi

Tangawizi pia ina faida nyingi katika mwili wako na afya yako. Tengeneza juisi robo lita yenye mchanganyiko wa tangawizi, komamanga na asali. Kunywa mchanganyiko huo kutwa mara 2 au 3 kwa matokeo ya haraka.

Namna nyingine ni kuchukua kijiko kikubwa kimoja cha juisi ya tangawizi (majimaji ya tangawizi) changanya na kijiko kikubwa kimoja cha asali na vijiko vikubwa 2 vya mbegu kavu za uwatu na uuache mchanganyiko huu kwa usiku mmoja. Kunywa mchanganyiko huu kesho yake ili kuondoa sumu kwenye mapafu yako.



MAFUTA YA MHARADALI

Mustard Oil

Chukua mafuta kidogo ya mharadali na uchanganye na kafuri (camphor) ndani yake. Jipakae mchanganyiko huu taratibu sehemu yote ya kifua mpaka uone nafuu inajitokeza. Hakikisha unayapasha mafuta kidogo katika moto kabla ya kuanza kujipaka taratibu (masaji) ili kifua kiweze kuhisi au kulipata hilo joto na hatimaye upate uponyaji kwa aharaka zaidi. Fanya zoezi hili wiki 2 hadi 3


MTINI

Mtini ni dawa nyingine ya asili (home remedy) nzuri dhidi ya pumu. Loweka baadhi ya mitini mikavu ndani ya maji kwa usiku mmoja. Kula huo mtini uliolowekwa kesho yake asubuhi kabla ya kula kitu kingine chochote. Pia kunywa maji hayo yaliyoloweka mtini kwa ajili ya kujitibu pumu au asthma. Fanya hivi kwa wiki 2 hadi 3

 CORDYCEPS PLUS CAPSULES

Availability : In Stock
Ingredients: Cordyceps sinensis mycelium, Radix ginseng

Characteristics and Benefits:

Improves immunity against attacks of microorganisms;
Possess anti-cancer property;
Enhances functions of liver, lungs and kidney;
Provides energy for those who suffer from chronic fatigue.
Suitable for:

People with compromised immunity
People with weakened functioning of liver, lungs, or kidney
People with asthma
Seniors with decreased general wellbeing
People with chronic fatigue
Athletes with increased demand

MAFUTA YA MKALITUSI

Mafuta ya mkalitusi (Eucalyptus essential oil) yanaweza kupelekea uponyaji wa haraka kwa mtu anayesumbuliwa na pumu. Weka matone machache ya mafuta haya ndani ya kikombe cha maji ya moto na usogeze pua yako karibu na mvuke unaojitokeza na uuvute ndani taratibu. Hii itasaidia kuzifungua pua zilizokuwa zimeziba sababu ya pumu na hivyo hewa inaweza kuanza kuingia na kutoka kirahisi zaidi.



ASALI

Asali

Kama unatafuta dawa ya asili ya kutibu pumu basi asali ndiyo dawa bora ya asili inayotibu pumu kuliko dawa nyingine yoyote. Unaweza kutumia kijiko kidogo kimoja cha chai kilichochanganywa na robo lita ya maji ya moto walau mara 2 mpaka 3 kwa siku au unaweza kuwa unanusa ile harufu fresh ya asali mara kadhaa kila siku.

Namna nyingine ni kuchukua kijiko kikubwa kimoja cha asali mbichi changanya na nusu kijiko kimoja cha chai cha mdalasini ya unga na ulambe mchanganyiko huo kila unapoenda kulala kila siku hadi upone.

KITUNGUU MAJI

Vitunguu vinajulikana kuwa na sifa ya kutibu uvimbe (inflammatory) na vimethibitika kuwa na msaada mkubwa katika kusafisha njia ya hewa. Kwahiyo kama wewe ni mhanga wa pumu au asthma basi unapaswa kuwa unatumia vitunguu maji kwa wingi kila siku vikiwa vibichi kabisa, vikiwa katika kachumbali au hata vikiwa vimepikwa pamoja namboga mboga zingine.



MATUNDA PORI NA LIMAO

Matunda kama stroberi, bluberi, papai, na machungwa yameonyesha kuwa na msaada kwa watu wanaosumbuliwa na pumu. Pia limau zina vitamin C na zinatakiwa kutumia sambamba na maji, sukari/asali na chumvi kidogo ya mawe walau mara moja kwa siku kwa majuma kadhaa ili kujitibu ugonjwa huu wa pumu.


SAMAKI

Kula mara kwa mara samaki kama ‘salmon’ (au samoni kwa Kiswahili ni samaki mkubwa mwenye mnofu mwekundu), tuna au jodari, dagaa chumvi wa baharini (sardines) kunaweza kuwa msaada mkubwa sana katika kujitibu tatizo la pumu. Samaki hawa wote huyafanya mapafu yako kuwa safi, salama na yenye nguvu katika kupambana na tatizo la pumu na kuitibu haraka na kwa ufanisi. Ingawa ikiwa hauwezi kula hawa samaki katika hali ya kupikwa basi unaweza kubadili kwa kutumia mafuta yatokanayo na samaki hawa.



ZABIBUBATA/ZABIBU NYEKUNDU

Zabibubata ni nzuri sana katika kutibu pumu. Ponda ponda zabibubata kadhaa na ongeza asali kidogo ndani yake, tumia mchanganyiko huu kila siku na ukae mbali na pumu.

KUDING PLUS TEA

Characteristics and Benefits:

Prevents common cold and flu;
Alleviates rhinitis, itching eyes, red eyes and pain in the eyes caused by wind-heat;
Detoxifies and improves healthy bowel movement;
Improves mental focus and memory;
Accelerates blood circulation, reduces blood cholesterol, blood sugar and blood pressure;
Prevent deterioration of heart and brain function;
Maintains proper body weight.
Suitable for:

All groups except for pregnant women



SHAMARI

Tumia mbegu za shamari kila mara ili kujitibu na shambulio la asthma/pumu

MAZIWA YA MOTO
Ongeza kiasi sawa cha mafuta ya mzeituni na asali ndani ya kikombe cha maziwa ya moto. Kunywa mchanganyiko huu pamoja na punje mbili au tatu za kitunguu swaumu kabla ya chakula cha asubuhi kwa majuma kadhaa. Dawa hii ya asili inaponya pumu kwa haraka sana.

MAJANI YA KOTIMIRI(PARSLEY LEAF)
Majani ya kotimiri (Parsley leaf) ni dawa mbadala nzuri sana kwa ajili ya kikohozi. Andaa chai ya majani haya na asali unywe kila siku. Itatibu kikohozi, itasafisha koo na kutibu pumu kadri siku zinavyosogea wakati ukiendelea kutumia chai hii kila siku

Mpendwa msomaji nashukuru Kwa kuchukua muda wako kufatilia makala zangu za afya nasema ASANTE NA MUNGU AKULIPE KHERY PIA IKIWA UNA MAONI AU USHAURI NIANDIKIE UJUMBE  KUPITIA KATIKA EMAIL AU NAMBA ZANGU HAPO CHINI

KUSOMA ZAIDI MAKALA MBALIMBALI  ZA AFYA TEMBELEA
 NAYTHAMHEALTHCARE.BLOGSPOT.COM

 ~Makala hii imeandaliwa na Dr Naytham Salum
E-mail nsalum998@gmail.com
+255623026602/+255746465095

PLZ USISAHAU KUSHARE, KUKOMENT, KULIKE NA WATAG RAFIKI ZAKO WAJIFUNZE

Jumamosi, 7 Januari 2017

TIBA SAHIHI YA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME

FAHAMU TIBA YA TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME

Asalaam alaykum warhmatullah wabarakatul ndugu mpenzi msomaji  katika zama hizi za sayansi na teknolojia tatizo la kupungua nguvu za kiume limekuwa kubwa sana, siyo Tanzania tu, bali duniani kote,
 Jambo muhimu analopaswa mwanaume yeyote kufahamu ni kwamba, kupungua nguvu za kiume siyo ugonjwa, ni dalili ya ugonjwa na  Hii ina maana kuna dosari au udhaifu wa kiutendaji ndani ya mwili wake,
 
SABABU ZA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME
Kuna sababu zaidi ya 250 zinazosababisha mwanaume apungue nguvu za kiume,Mtu anaweza kujiuliza kwa nini kuwe na sababu nyingi namna hiyo

MAANA YA NGUVU ZA KIUME
Nguvu za kiume ni jina la jumla lenye vipengele vingi ndani yake ikiwa ni pamoja na hamu ya mapenzi; kusimama kwa uume barabara kuchelewa kufika kileleni kiasi cha kufurahia tendo la ndoa; uwezo wa kurudia tendo la ndoa; pumzi, wepesi na uchangamfu wa mwili katika kutenda tendo la lenyewe.

Ni viungo gani vinavyohusika na nguvu za kiume?
Nguvu za kiume ni tukio pana sana lenye kuhusisha viungo na vitu vingi ndani ya mwili. Kuna zaidi ya viungo na vitu 50 ndani ya mwili wa mwanaume vinavyohusika na nguvu za kiume ambapo viungo hivi pia hufanya kazi zingine za mwili. Baadhi ya viungo hivyo ni ubongo, moyo, mishipa ya neva mishipa ya ateri, mirija iliyo ndani ya uume iitwayo corpora cavernosa.

Viungo vingine ni neva maalumu za parasympathetic, tezidume (prostate gland), ini, figo, homoni ya testestorone, kemikali za  acetylcholine, serotonin, na dopamine, uti wa mgongo, eneo la chini ya mgongo (kiuno), eneo la nyonga.

Viungo vingine ni misuli maalumu iitwayo pelvic floor, tezi pituitari (pituitary gland), utando maalumu wa uumeni uitwao tunica albuginea, misuli iitwayo pubococcygeus [PC muscles], kemikali ya nitric oxide, kemikali ya prolactin n.k.

Nini maana ya kupungua nguvu za kiume?
Unapopungua nguvu za kiume ina maana ndani ya mwili wako kuna baadhi ya vitu katika vitu nilivyovitaja hapo juu havifanyi kazi vizuri ipasavyo na inavyotakiwa. Yawezekana ni figo ndilo halifanyi kazi vizuri, au ini, au tezi dume, au neva ya parasympathetic, au moyo una tatizo au mishipa ya ateri, au misuli ya pelvic au homoni fulani iko juu sana au iko chini sana (hormonal imbalance), orodha ni ndefu sana.

Kitendo cha baadhi ya viungo hivyo kutofanya kazi vizuri basi hapo hutokea upungufu katika nguvu za kiume. Upungufu huo unaweza kuwa ni:

1. Kukosa hamu ya mapenzi;

2. Uume kusimama kwa uregevu;

3. Kuwahi kufika kileleni;

4. Kuchelewa sana kufika kileleni ( kushindwa kufika kileleni kabisa);

5. Kushindwa kurudia tendo la ndoa;

6. Kuhisi maumivu wakati wa tendo la ndoa au baada ya tendo hilo;

7. Kukosa pumzi na uchangamfu wa mwili katika utendaji;

8. Kuchoka sana baada ya tendo la ndoa na hata kukinai kabisa au hata kusikia kichefuchefu;

Mpendwa  msomaji, ili uelewe vizuri zaidi labda niseme kwamba, nguvu za kiume ni kiwanda; na ni zaidi ya kiwanda. Ndani ya kiwanda kuna umeme, maji, madawa, watu (wafanyakazi wa kila taaluma na fani), mashine, mitambo n.k.

Ikitokea kitu kimojawapo kukosekana, mathalani umeme, au wafanyakazi wakagoma, au kukakosekana madawa muhimu au maji na kadhaa wakadha, basi bidhaa inayotarajiwa kupatikana sokoni, kwa hakika haitapatikana.

Vivyo hivyo nguvu za kiume, mathalani, ikitokea tezidume kutofanya kazi vyema, basi hapo mwanaume hatoona nguvu za kiume, zitapungua au zitaisha kabisa!

Kwa hiyo upungufu wa nguvu za kiume ni upungufu au kasoro za kiutendaji wa viungo ndani ya mwili wa mwanaume. Mwanaume yoyote anapaswa kutambua jambo hili.

Lakini nini kinachopelekea viungo hivyo vishindwe kufanya kazi vizuri?
Kuna maradhi kadhaa, vyakula tunavyokula, tabia na mtindo wa maisha vinavyoweza kupelekea viungo hivyo kutofanya kazi vizuri. Baaadhi ya maradhi hayo na tabia hizo ni kujichua/punyeto (masturbation); kisukari; presha ya kupanda; presha ya kushuka; uvutaji wa sigara; unywaji wa pombe; madawa ya kuleva; kufanya kazi kupita kiwango na kukosa muda wa kupumuzika; matatizo ya kukosa usingizi na kuchelewa kulala usiku.

Sababu zingine za kupungua nguvu za kiume ni kutokunywa maji ya kutosha, tatizo la kufunga choo hasa pale unapotumia nguvu nyingi kusukuma choo; kutofanya mazoezi; ukosefu wa kumbukumbu; uzito mkubwa/unene mkubwa; kitambi; kuvimba kwa tezidume (Benign Prostate Hyperplasia).

Sababu zingine ni saratani ya tezi dume (Prostate cancer), matibabu ya mionzi ya tezidume na upasuaji, ugonjwa unaoathiri vitendo na shughuli za mwili kama vile mwondoko na balansi (multiple sclerosis), ugonjwa ambao hudhuru mawasiliano ya ubongo na miondoko ikiwa ni pamoja na kutembea, kuongea na kuandika (parkinson’s disease), vyakula vya mafuta, vyakula vilivyowekewa homoni bandia za kike n.k.

Sababu zingine ni maumivu ya mgongo/kiuno; baadhi ya madawa ya kemikali (madawa ya hospitali); kiharusi (stroke); upungufu katika utendaji wa kazi za gonadi (hypogonadism); uzalishaji mwingi wa homoni ya thyroid.

Sababu zingine ni kutozalishwa kwa homoni ya thyroid ya kutosha; ugonjwa unaoathiri uzalishaji wa homoni ya cortisol (cushing’s syndrome); ugonjwa wa kupinda uume (peyronie’s disease); kukakamaa kwa mishipa ya damu (atherosclerosis); orodha ni ndefu sana, ni zaidi ya 200.

Hivyo mwanaume anapopungua nguvu za kiume, ina maana kuna ugonjwa ndani ya mwili wake, au unaweza kuwa huo ugonjwa umeshadhihirika (umeshatokeza) kwa nje, au huo uko ndani ya mwili unamla na kummaliza kimyakimya kama yalivyo baadhi ya magonjwa ambapo baadaye hulipuka. Hii ndiyo maana kitaalamu tunasema kupungua nguvu za kiume siyo ugonjwa ni dalili ya ugonjwa. Unapopungua nguvu za kiume hiyo ni KENGELE YA TAHADHARI kwamba ndani ya mwili wako kuna kitu hakifanyi kazi vyema. Hivyo, unaambiwa kuchukua TAHADHARI kabla ya HATARI!

KOSA KUBWA WANALOFANYA WANAUME WENGI!
Wanaume wengi wanapopungukiwa nguvu za kiume hukimbilia kutafuta dawa za kuongeza nguvu za kiume, na siyo kutibu. Hili ni KOSA KUBWA sana!

Ni kosa kubwa kukurupuka kubugia dawa za nguvu za kiume bila kujua chanzo cha tatizo na bila kujua hiyo dawa inakwenda kutibu tatizo gani. Kwa njia hiyo, utamaliza miaka hata zaidi ya 100 na hata miaka elfu moja na hautapona!

Upungufu wa nguvu za kiume lazima utibiwe kuanzia chanzo cha tatizo; kwa maana ya kwamba mzizi wa tatizo sharti ung'olewe kwanza! Mathalani, kama tatizo ni la homoni ijulikane kwanza; kama ni tatizo la tezi ijulikane kwanza, kisha matibabu sahihi yaelekezwe katika maeneo hayo. Hayo ndiyo matibabu, na si vinginevyo. Angalia mwenyewe, upungufu wa nguvu za kiume unaweza kutokana na kisukari kwa mwanaume huyu, au shinikizo la damu la kupanda (HIGH BLOOD PRESSURE) kwa mwanaume yule; au shida ya tezidume kwa mwanaume mwingine au shida ya kihomoni (HORMONAL IMBALANCE) kwa wanaume  wengine, basi vipi iingie akilini kwamba wote hao watatibiwa na dawa aina moja? Watu wengi wengi wameelewa kimakosa sana ndiyo maana hata matibabu yamekuwa ni tatizo kubwa sana.

Nani anaweza kutibu nguvu za kiume?
Kuna watu wengi sana hivi leo wanaodai kutibu nguvu za kiume. Ukweli wa mambo ni kwamba siyo kweli! Ni watu wachache sana wana uwezo wa kutibu tatizo la kuishiwa nguvu za kiume. Utakuta mtu anatangaza dawa ya aina moja kuwatibu watu wote wenye matatizo ya nguvu za kiume. Tabia hii pia imejengeka kwa baadhi ya watu, hupiga simu na kuuliza moja kwa moja, "Daktari, dawa za nguvu za kiume ni shilingi ngapi?"

 Kila mwanamume ana sababu na chanzo chake cha kupungua nguvu za kiume. Kama wanaume 100 waliopungukiwa nguvu za kiume watajipanga mstari, kila mmoja atakuwa na sababu yake na chanzo chake cha kupungukiwa nguvu za kiume tofauti kabisa na mwingine.

Hii humaanisha kila mgonjwa atakuwa na dawa yake ya kipekee kabisa tofauti na mwingine. Sasa itashangaza kuona huyu kapungukiwa nguvu za kiume kutokana na mishipa ya ateri kutofanya kazi vizuri, na yule kapungukiwa nguvu kutokana na kuvimba kwa tezidume,Halafu wote wapate dawa aina moja! Hiki ndicho kinachofanyika na watu wengi wamepoteza pesa na muda kwa matibabu yasiyokuwa na maana.

Yahitajika daktari mtaalamu aliyebobea katika mfumo wa uzazi wa mwanaume na mfumo wa mkojo, ndiye anayeweza kutibu tatizo la nguvu za kiume. Yaani, daktari ambaye anajua vizuri ndani na nje utendaji wa figo, ini, moyo n.k; awe ni daktari wa tiba asilia au daktari wa tibakemikali (yaani daktari wa hospitali) siyo kila mtu tu au kila daktari. Hata kama utakwenda kwenye hospitali kubwa yoyote duniani unayoijua, na ukagonga hodi katika chumba cha daktari, ukamwambia, "Nina tatizo la upungufu au kuishiwa nguvu za kiume," atakurifaa kwa daktari maalumu aliyebobea katika mfumo wa uzazi wa mwanaume na mfumo wa mkojo. Hata kwa madaktari wa tiba asilia, hali ni hivyo hivyo, lazima ukutane na ambaye amebobea katika mfumo wa uzazi wa mwanaume.
Kwa sababu unapotibu nguvu za kiume unakuwa unatibu viungo vya mwili kwa ujumla. Daktari aliye mtaalamu anakuwa ana uwezo wa kutambua tatizo la kiungo kilichokorofisha mwilini kutokana na kumhoji mgonjwa; na anaweza kwenda mbali zaidi kwa kujiridhisha kwa vipimo.

LISHE MUHIMU KUREJESHA NGUVU ZA KIUME
wakati mwingine mwanamme hupatwa na tatzo la Nguvu Za Kiume kutokana na kukosa madini lishe muhimu yanayohitajika mwilini mwake
Naam tuangalie viinilishe (nutrients) na madini yanayohitajika katika mwili wa mwanaume ili mwanaume huyo awe lijali na mwenye nguvu za kiume za kutosha.

Antioxidant Nutrients

Upungufu wa vitamin E, vitamin C na selenium huwa na athari kwenye uzalishaji na uogeleaji wa shahawa (sperm motility). Tafiti zimeweza kuonyesha kwamba vitamin E kiasi cha vipimo vya kimataifa (International Units - IU) 100-200 kwa siku huboresha afya ya shahawa za mwanume asiyeweza kumzalisha mwanamke (infertile man) na kumwongezea uwezekano wa kumtia mimba mwanamke. Kadhalika vitamin C huongeza wingi wa mbegu za kiume kwenye shahawa (sperm count) na uwezo wa shahawa kuogelea ndani ya uke wa mwanamke (sperm motility). Tafiti pia zimeonyesha kwamba selenium husaidia uogeleaji wa shahawa.

Mahitaji (Recommended Dietary Allowances – RDA) ya vitamin C ni miligramu 90. Mwanaume anayevuta sigara anahitaji miligramu 125. Vyakula vyenye vitamin C ni pamoja na matunda jamii ya machungwa (citrus fruits), cantaloupe, kiwi, maembe, strawberries, broccoli, cauliflower, pilipili nyekundu na juisi ya nyanya. Vitamin E RDA ni 15 IU (natural source) na 22 (synthetic). Vyakula muhimu ni pamoja na ngano, karanga na jamii zake, mafuta ya mimea, mbegu zisizokobolewa (whole grains). Selenium RDA ni 15 micrograms. Vyakula muhimu vyenye selenium ni pamoja na samaki, seafood, kuku, organ meats, whole grains, karanga na jamii zake (nuts), vitunguu, uyoga, vitunguu swaumu.

Vitamin B12

Upungufu wa vitamin B12 hupelekea lower sperm counts na impaired sperm motility. Vyakula muhimu vyenye B12 ni pamoja na nyama, kuku, samaki, maziwa na bidhaa zake, mayai, soya na maziwa ya mchele (rice milk).

Zinc

Madini ya zinc ni muhimu sana kwa masuala ya uzazi na uzalishaji wa shahawa. Wanaume wenye matatizo ya uzazi wana upungufu wa madini ya zinc. Upungufu wa madini hayo pia hupelekea wanaume kuwa na kiasi kidogo cha homoni za kiume (low testosterone levels). Wanaume wenye shida hiyo wakipewa madini ya zinc huwa na ongezeko la mbegu za kiume (increased sperm counts) na uwezo wa kutia mimba. RDA ya zinc ni miligramu 11 kwa siku (wanawake huitaji miligramu 8). Vyakula muhimu ni pamoja na pweza na chaza, dark turkey meat, lentils, ricotta cheese, tofu, yogurt, spinach, broccoli, green beans, na juisi ya nyanya. Hakikisha kwamba pamoja na madini ya zinc pia unapata madini ya copper kiasi cha miligramu moja kwa siku kwa kuwa madini hayo hufanya kazi kwa pamoja kwa kutegemeana.

L-carnitine

Husaidia kuongeza sperm count. Utafiti mmoja uliofanywa ulibainisha kwamba gramu 3 kwa siku za L-carnitine kila siku kwa muda wa miezi mitatu uli-saidia kuongeza sperm count na sperm motility kwa wanaume 37 kati ya 47. L-carnitine hupatikana kwenye nyama na maziwa

NOTED;KABLA YA MATUMIZI YA DAWA YA KUONGEZA NGUVU ZA KIUME NI VYEMA UKAWASILIANA NA DAKTARI WAKO WA KARIBU ILI KUPATA USHAURI ZAIDI

Asante kwa kuwa nami kupata elimu hii rafiki kama una maswali/maoni au mapendekezo yoyote niandikie kupitia namba na email yangu hapo chini

KUSOMA ZAIDI MAKALA MBALIMBALI ZA AFYA TEMBELEA NAYTHAMHEALTHCARE.BLOGSPOT.COM

Makala hii imeandaliwa na Dr Naytham S Masoud
Email-nsalum998@gmail.com
+255623026602/+255746465095

PLZ USISAHAU KUSHARE, KULIKE NA WATAG RAFIKI ZAKO WAPATE KUJIFUNZA

Jumamosi, 19 Novemba 2016

UGONJWA WA KUOTA KINYAMA SEHEMU YA HAJA KUBWA/BAWASIRI (HEMORRHOIDS)

FAHAMU UGONJWA WA BAWASIRI AU KUOTA KINYAMA SEHEMU YA HAJA KUBWA (HEMORRHOID) NA NAMNA YA KUEPUKA NA UGONJWA HUU

Asalaam alaykum warhmatullah wabarakatul, sifa njema anastahiki Allah Subuhhanah'wataala Kwa afya na uzima alotujaalia,
Leo tena napenda kuzungumzia ugonjwa wa Bawasiri/hemorrhoids)
Naam watu wengi wanasumbuliwa na tatizo hili ambalo huwafanya kuwa na uoga na aibu wa kuelezea na kushindwa hata kwenda hospital kupata tiba idadi yake inazidi kuongezeka

BAWASIRI/HEMORRHOIDS
Ni ugonjwa unaotokana na kuathirika kwa mishipa ya damu ya ndani na nnje ya sehemu ya haja kubwa na wakati mwingine mishipa hiyo huweza kupasuka/kuteleza na kuvuja damu kwenye njia ya haja kubwa na kasababisha kutoka kinyama au uvimbe
Ugonjwa huu wa bawasiri kwa lugha ya kitaalamu tunauita HEMORRHOIDS ilhali kwa lugha ya kingereza unafahamika kama piles
~tatizo hili huwaathiri watu wote ila zaidi huwaathiri watu wazima kuliko watoto na inakadiriwa kuwa karibu 50%ya watu wote wako katika hatari ya kupata tatizo hili katika umri wa miaka 30_50

AINA ZA BAWASIRI
~Kuna Aina mbili za bawasiri
(A) BAWASIRI YA NDANI
~Aina hii ya bawasiri hutokea ndani ya mfereji wa haja kubwa huwa haiambatani na maumivu na wengi huwa hawajitambui kuwa Wana tatizo hili
~Aina hii hutokana na kuvimba na kuharibika kwa mshipa wa artery za ndani ya mfereji wa haja kubwa
~Aina hii imegawanyika katika madaraja manne

(1)DARAJA LA KWANZA ~Hii ni bawasiri ambayo haitoki mahal pale panapohusika

(2)DARAJA LA PILI ~hii  hutokea wakati wa haja na kurudi yenyew ndani baada ya kujisaidia

(3)DARAJA LA TATU :hii hutokea wakati wa haja kubwa na mtu kuweza kurudisha ndani yeye mwenywe

(4)DARAJA LA NNE :hii ni bawasiri inayotoka na huwa ngumu kurudi

(B)BAWASIRI YA NNJE
~Aina hii ya bawasiri hutokea katika eneo la mwisho kabisa la mfereji wa haja kubwa na huambatana na maumivu makali na kuwashwa kwa ngozi katika eneo la tundu Hilo pia husababisha mishipa ya damu (vena) kupasuka na damu kuganda na kasababisha Aina ya bawasiri iitwayo THROMBOSED HEMORRHOIDS

CHANZO CHA TATIZO
~chanzo halisi cha ugonjwa huu hakijapatikana ila Kuna vitu ambavyo huwa chanzo cha kupata ugonjwa wa bawasiri ambayo ni ÷
👉KUFANYA MAPENZI KINYUME NA MAUMBILE
👉KUHARISHA KWA MUDA MREFU
👉TATIZO LA KUTOPATA CHOO VIZURI
👉MATATIZO YA UMRI
👉KUKAA KITAKO KWA MUDA MREFU
👉UZITO KUPITA KIASI
👉MATUMIZI YA VYOO VYA KUKAA KWA MUDA MREFU

DALILI ZA BAWASIRI
dalili za ugonjwa wa Bawasiri ni :

👉Ngozi kuwasha katika eneo la tundu la haja kubwa
👉kupata maumivu makali wakati wa kujisaidia
👉kutokea uvimbe katika eneo la tundu la haja kubwa
👉kujitokeza kwa kinyama katika eneo la tundu Hilo
👉kinyesi kuwa na damu na kunuka harufu mbaya sana

VIPIMO NA UCHUNGUZI
Vifuatavyo ni vipimo vinavyotumika kugundua ugonjwa wa Bawasiri
Digital rectal examination
Kipimo cha njia ya haja kubwa (Proctoscope)
Kipimo cha utumbo mpana (Sigmoidoscope)

MATIBABU

Matibabu ya mwanzo ya ugonjwa huu  kawaida huwa ni ongezeko la kula chakula kilicho na faiba(high fibre) na  vinywaji Kwa wingi ili kudumisha haidresheni pia  dawa za kutibu maambukizi  husaidia kwa maumivu na mapumziko
Lakini pia kuna  Baadhi ya taratibu kubwa zinaweza kutekelezwa ikiwa dalili ni kali au hazistawi kwa mwelekeo wa matibabu ya awali
Mfano wa taratibu hizo ni :
(1)Rubber band ligation - Hapa mishipa hufungwa na rubber band ili kuzuia damu kwenda kwenye eneo liloathirika, na hutumika kwenye aina ya ndani ya bawasiri.

(2)Sclerotherapy- Hapa kemikali huwekwa kwa njia ya sindano
Coagulation (infrared, laser and bipolar)

(3)TCM MEDICAL-hapa Mgonjwa hushauriwa kutumia Dawa Aina ya TCM  kulingana na ukubwa wa tatizo Lake ambazo husaidia kurahisisha mfumo wa mmeng'enyo na kuponya chanzo cha tatizo
Mfano wa Dawa hizo ni
(1)MEAL CELLULOSE TABLET 700MG
/MEAL CELLULOSE OR DIETARY FIBER. Meal cellulose,also referred to dietary fiber,includes all parts of plant foods that the body can not digest or absorb. Therefore, it passes relatively intact through our stomach,small intestine,colon and out of our body.


(2)SPIRULINA PLUS CAPSULE 500MG
is a  natural “algae” (cyanbacteria) powder that is incredibly high in protein and a good source of antioxidants, B-vitamins and other nutrients. When harvested correctly from non-contaminated ponds and bodies of water, it is one of the most potent nutrient sources available



(3)PARASHIELD CAPSULES 500MG
(4)ALOE VERA PLUS CAPSULE 500MG

Upasuaji;
         Hemorrhoidectomy
         Stapled hemorrhoidopexy
Ni hatua ya mwisho iliyotengwa Kwa wale wanaokosa mabadiliko ingawaje sio nzuri kiafya Kwa ujumla

NJIA ZA KUZUIA BAWASIRI

badilisha mfumo wako wa chakula,
Kula High fibre diet(vyakula vyenye nyuzinyuzi  kama mboga za majani, matunda, na nafaka kwa wingi.

Kunywa maji mengi kwa siku (glasi sita had nane kwa siku)

Punguza kukaa kwa muda mrefu sana hasa ukiwa chooni, kwa sababu unaweza kuongeza shinikizo katika mfereji wa haja kubwa

Fanya mazoezi mepesi na sio mazoezi magumu

MADHARA YA TATIZO LA BAWASIRI ugonjwa wa Bawasiri usipotibiwa huleta athari zifuatazo Kwa Mgonjwa
👉kupata upungufu wa damu (anemia)
👉Kupata tatizo la kutokuweza kuhimili choo
👉hupunguza nguvu za kiume na kuondoa hamu ya tendo la ndoa kwa wanawake kwasababu husababisha maumivu Kwa Mwanamke wakati wa tendo la ndoa
👉kuathirika kisaikolojia
👉kukosa moral ya kufanya Kazi kutokana na maumivu makali

NOTED:
NDUGU RAFIKI KAMA UNA UGONJWA HUU EPUKA KULA NYAMA NYEKUNDU NA PILIPILI PIA UNAWEZA  WASILIANA NAMI KWA USHAURI WA MATIBABU YA KUONDOA TATIZO HILI PASIPO KUFANYA UPASUAJI
Asante kwa kuwa nami kupata elimu hii rafiki kama una maswali/maoni au mapendekezo yoyote niandikie kupitia namba na email yangu hapo chini

KUSOMA ZAIDI MAKALA MBALIMBALI ZA AFYA TEMBELEA NAYTHAMHEALTHCARE.BLOGSPOT.COM

Makala hii imeandaliwa na Dr Naytham S Masoud
Email-nsalum998@gmail.com
+255623026602/+255746465095

PLZ USISAHAU KUSHARE, KULIKE NA WATAG RAFIKI ZAKO WAPATE KUJIFUNZA

Alhamisi, 17 Novemba 2016

SABABU ZA UKE KUTOA HARUFU MBAYA

FAHAMU SABABU ZA MWANAMKE KUTOA HARUFU MBAYA UKENI

Asalam alaykum warhmatullah wabarakatull
Ni matumaini nyote mnaendelea vyema, nami alhamdulillah ala kul Hali naendelea vyema
 Leo naona ni bora tukazungumzia tatizo la kutokwa na harufu mbaya ukeni maana watu wengi hudhani kuwa na harufu mbaya itokayo ukeni ni matokeo ya uchafu tu na ndio maana wanaume huwachamba wake zao kuwa hawajuhi kujisafisha na kufanya wanawake kuongeza jitihada katika kujisafisha ukeni,leo napenda kuzungumzia tatizo hili linalowasumbua wanawake wengi na kuwaumiza kichwa kutokana na kwamba lina athari kubwa sana kwani hufanya ndoa zao kudumaa NK,
~kitaalamu Hali ya mwanamke kutokwa na maji yenye rangi nyeupe au njano ni Hali ya kawaida na sio tatizo Lakini endapo maji yanatoka yapo katika Hali ya ute mzito wenye rangi nyeupe au kahawia na yanatoa harufu kali au kuwasha hapo una tatizo
~majimaji au ute unaoteleza kutoka sehemu za siri ni njia inayowezesha viungo vya uzazi vya mwanamke kujisafisha au kutoa uchafu wa seli zilizokufa na mabaki ya damu ya hedhi nnje ya mwili pia huvikinga viungo vya uzazi dhidi ya maaambukizi ya bacteria
~Kwa kawaida huwa hayatoi harufu na huwa hayawashi na huwa na rangi nyeupe au njano pia huwa na asidi ya LACTIN ambayo huzuia bacteria kuzaliana
~mwanamke hutoa kiasi cha grams 2 za seli zilizokufa kutoka kwenye mji wa kizazi na grams 3 za ute mwepesi kila siku, kiwango hicho kinaweza kuongezeka au kupungua kutegemeana na mzunguko wa hedhi pia Kuna wakati ute huwa mwepesi na unaovutika na Kuna wakati pia huwa mzito wa rangi ya njano hautoi harufu

VISABABISHI VYA TATIZO HILI
~sababu za kutokwa na uchafu ukeni una vyanzo vingi sana vifuatavyo ni vyanzo vya tatizo hili

(1)BACTERIA VAGINOSIS
~Chanzo halisi cha ugonjwa huu hakijafanikiwa kuwa wazi,kinachotokea ni kuongezeka kwa ghafla kwa idadi ya ya bacteria hawa na kubadilisha uwiano wa kawaida katika mazingira ya uke, wanawake wenye wapenzi wengi na wanaofanya mapenzi kwa njia ya mdomo Wana hatari ya kupata tatizo hili

(2)TRICHOMONAS
~maambukizi haya hutokana na Aina ya protozoa wa seli moja, trichomonas mara nyingi huambukizwa kwa njia ya ngono, protozoa huyo huweza kukaa kwenye unyevu unyevu kwa Muda wa saa 24 Bila kufa hivyo kufanya taulo na chupi zisizokauka kuwa chanzo kingine cha tatizo hili

(3)YEAST INFECTION
~kwa kawaida Kuna kiwango kidogo cha yeast (candida albicans) katika uke, huwa tunasema Kuna maambukizi pale kiwango kinapozidi Hali ambayo inatokana na kubadilika kwa Hali ya hewa ukeni (Change in the PH balance of vagina)
~maambukizi ya yeast hayatokani na tendo la ndoa na tendo la ndoa, mambo ambayo huchangia tatizo hili ni MATUMIZI YA DAWA ZA KUZUIA MIMBA, MAWAZO, UJAUZITO, KISUKARI NA MATUMIZI YA ANTIBIOTICS

(4)VAGINAL OR CERVICAL CANCER,
~mtu anapokua na kansa ya uke, hutokwa na maji ya harufu mbaya, hivyo ni heri uwe unafanya check up ili kujua Afya yako na kwakuwa cancer ya kizazi inapona hivyo ni vema ukatambua mapema uanze tiba

(5)SEXUAL TRANSMITTED DESEAS (STDs)~Kuna baadhi ya magonjwa kama vile KASWENDE NA KISONONO yanasababishwa na ngono na kuwa chanzo cha tatizo hili
(6)POOR HYGIENE ~tatizo la kutokwa na maji wakati mwingine husababishwa na muhusika kua mchafu yan mtu unaoga kwa siku mara moja, chupi moja ndio hiyo hiyo mwaka mzima, pads unakaa nayo saa 24, ukienda kukojoa ujitawadhi na maji masafi hivyo unategemea utakua salama kweli??? Zingatia usafi mrembo

DALILI ZA TATIZO HILI
~kutokwa na uchafu ukeni unaoambatana na kuwashwa au kutokewa na vipele, hii hutokana na kuharibika kwa uwiano wa bacteria hivyo kuwa na madhara na uchafu hutoka wa aina tofauti hapa chini nitaelezea kila Aina ya uchafu na dalili zake
@UCHAFU WENYE RANGI YA KAHAWIA AU DAMU
~huu uchafu huonyesha dalili ya kuwa mzunguko wako wa hedhi umevulugika na wakati mwingine ni dalili ya kansa ya kizazi, mwanamke anayepata tatizo hili hutoa damu nyingi kuumwa sana nyonga
@UCHAFU WENYE RANGI YA NJANO /KIJANI WENYE HARUFU MBAYA
~Endapo uchafu huo utatoka kama povu na wenye rangi ya kijani au njano na ukiambatana na harufu mbaya huwa ni dalili ya ugonjwa wa trichomonas, maambukizi ya parasite yanatokana na ngono zembe, dalili Yake nyingine ni maumivu na kuwashwa wakati wa kutoa haja ndogo
@UCHAFU MWEUPE MZITO KAMA JIBINI
~mara nyingi hii huwa ni dalili ya maambukizi ya fangasi(YEAST INFECTION) na dalili nyingine huwa ni kuvimba sehemu ya nje ya siri, kuwashwa na kupata maumivu makali wakati wa tendo la ndoa
@UCHAFU MWEUPE/KIJIVU WENYE HARUFU YA SAMAKI
~uchafu wa Aina hii ni dalili ya maambukizi ya bacteria vaginosis, mara nyingi mwenye tatizo hili husikia muwasho na maumivu sehem ya nnje ya uke

~MAMBO MUHIMU YA KUZINGATIA KUEPUKA TATIZO HILI NA TIBA YAKE
~Matibabu ya tatizo hili hufanyika baada ya kugundua chanzo cha tatizo na mara nyingi tiba Yake ni tiba ya dawa za antibiotics kitu ambacho si tiba nzuri zaidi kwasababu tatizo huweza kujirudia kila wakati na kusababisha matatizo zaidi hivyo tiba nzuri ni kuepuka hili tatizo kwa kufanya yafuatayo
👉EPUKA KUJIINGIZA VIDOLE MARA KWA MARA UKENI
👉EPUKA MATUMIZI YA DAWA ZA ANTIBIOTICS MARA KWA MARA
👉PUNGUZA KULA VYAKULA VYENYE SUKARI NYINGI
👉TUMIA PADS ZENYE ANIONS NI SALAMA KWA AFYA YAKO
👉SAFISHA VIZURI NGUO ZAKO ZA NDANI NA UZIANIKE JUANI NA HATA KUZIPIGA PASI
👉KUNYWA JUICE YA APPLE,STRAWBERRY, NANASI KWA WINGI
👉EPUKA KUFANYA NGONO ZEMBE
👉HAKIKISHA UNAJISAFISHA KILA UNAPOMALIZA KUJISAIDIA
👉EPUKA KUTUMIA DAWA ZA KUZUIA MIMBA
👉EPUKA KUTUMIA SABUNI AU VITU VYA MANUKATO UKENI,
NOTED :wanawake wengi mnapenda kutumia baadhi ya dawa kwa lengo la kuongeza vionjo  kwenye mapenzi pia kufanya uke kunukia vizuri, au kukaza uke rafiki uke una harufu nzuri sana ambayo haipatkan kokote hivyo haihitaji kuwekwa pafyumu Wala kusafishwa kwa sabuni za kemikali kwani huwa panajisafisha hivyo ni heri ukaacha kutumia kwani madhara Yake hayaonekani sasa ila baada ya Muda huonekana


Mpendwa msomaji nashukuru Kwa kuchukua muda wako kufatilia makala zangu za afya nasema ASANTE NA MUNGU AKULIPE KHERY PIA IKIWA UNA MAONI AU USHAURI NIANDIKIE UJUMBE  KUPITIA KATIKA EMAIL AU NAMBA ZANGU HAPO CHINI

KUSOMA ZAIDI MAKALA MBALIMBALI  ZA AFYA TEMBELEA
 NAYTHAMHEALTHCARE.BLOGSPOT.COM

 ~Makala hii imeandaliwa na Dr Naytham Salum
E-mail nsalum998@gmail.com
+255623026602/+255746465095

PLZ USISAHAU KUSHARE, KUKOMENT, KULIKE NA WATAG RAFIKI ZAKO WAJIFUNZE

UGONJWA WA FANGAS UKENI (VAGINAL CANDIDIASIS)

FAHAM NAMNA YA KUJITIBU NA KUJILINDA DHIDI YA UGONJWA WA FANGASI UKENI (VAGINAL CANDIDIASIS)

Asalaam alaykum warhmatullah wabarakatul ndugu msomaji wa page hii,kutokana na kupokea maoni na maswali yenu leo nimependa kuzungumzia ugonjwa wa fangasi ukeni ambao ni common hususani kwa wanawake,

Maambukizi ya fangasi sehemu za siri imekua ni tatizo kubwa sana Duniani 75%ya wanawake wote Duniani wanasumbuliwa na tatizo hili,na maambukizi haya ya fangasi  husababishwa na fangasi aina ya CANDIDA ALBICANS lakini pia maambukizi haya hujulikana kama YEAST INFECTIONS /THRUSH

CANDIDA ALBICANS hupatikana katika midomo, mpira wa kupitishia Chakula (PHARYNX), kibofu cha mkojo, uume au katika uke
bacteria Hawa huishi katika sehemu hizo Bila kuleta madhara, isipokua pale mazingira ya eneo husika, yanapobadilika, MFANO mabadiliko katika Hali ya PH
tutambue PH ya mwanamke ndani ya uke ni 4.0_4.5 au uwiano wake na vimelea (microorganisms) wengine, hivyo huharibiwa kutokana na sababu mbalimbali kama vile MATUMIZI YA MADAWA YA ANTIBIOTICS eg AMPICILLINE, CIPROFLAXINE, AMOXYLINE, DOXYCYCLINE, ERTHROMYCINE, NK pia kupungua kwa Kinga kutokana na magonjwa mbalmbal nk

maambukizi ya fangasi ukeni yamegawanyika katika sehemu KUU mbili nazo ni ÷
(1)MAAMBUKIZI YASIYO MAKALI (UNCOMPLICATED THRUSH)
~katika aina hii mgonjwa hupatwa na maambukizi Mara moja hadi nne kwa mwaka pia Dalili zake huwa si za kuogopesha na maambukizi haya husababishwa na fangasi aina ya CANDIDA ALBICANS

(2)MAAMBUKIZI MAKALI (COMPLICATED THRUSH)
Katika kundi hili mgonjwa hupatwa na maambukizi Zaidi ya Mara nne au Zaidi kwa mwaka pia Dalili zake huwa ni za kuogopesha kama maambukizi yatakua yametokea kipindi cha UJAUZITO, ugonjwa wa VVU, ugonjwa wa sukari nk

VIHATARISHI VYA MAAMBUKIZI YA FANGASI KATIKA UKE
~Mabadiliko ya mfumo wa homoni mwilini ambazo husababisha mabadiliko katika sehemu za siri
~magonjwa ya saratani ya tezi koo la Chakula (thyroid cancer)
~wanawake wenye umri wa miaka 20_30 wapo katika hatari ya kupata maambukizi haya wakati wale ambao wameshaacha kupata hedhi (menopause) na wale ambao hawajaanza kupata hedhi hawako katika hatari kutokana na mazingira na vitu wanavyotumia
~upungufu wa Kinga mwilin kutokana na magonjwa hatar ya saratani, kisukari, ugonjwa wa mononucleosis nk
~matumizi ya vidonge vya majira
~msongo wa mawazo
~kujamiana kwa njia ya kawaida Mara tu baada ya kujamiiana kupitia haja kubwa (anal sex)
~matumizi ya glycerin wakati wa kujamiiana husababisha maambukizi pia
~kuwa na historia ya kupata matibabu ya homoni (hormonal replacement therapy)
~ujauzto (husababisha kubadilika kwa mfumo wa homoni mwilini
~kuwa na utapiamlo (malnutrition
~kuvaa nguo za ndani ziszo kauka vzur
~kuvaa mavazi yanayoleta sana joto sehem za siri

DALILI ZA UGONJWA WA FANGASI UKENI
👉kuwashwa sehem za siri
👉kuhisi maumivu makali wakati wa kujamiiana (superficial dysapareunia)
👉kuhisi kuwaka moto sehemu za siri Mara baada ya kutoka kufanya tendo la ndoa au kutoka kukojoa (burning sensation
👉kupata vidonda ukeni (soreness
👉kuvimba na kuwa mwekundu katika mdomo wa nnje wa uke (labia minora
👉kupata maumivu wakati wa kukojoa
👉kutokwa na uchafu wa rangi nyeupe au kijivu unaoweza kuwa MWEPESI au MZITO au majimaji
NOTED :Dalili na viashiria hivi huwa mbaya Zaidi mwanamke anapokua mwezini

MATIBABU NA JINSI YA KUJIKINGA NA UGONJWA HUU WA FANGASI UKENI
Matibabu ya fangasi ya uke hutumia dawa za kuua fangasi (antifungals).  Mara nyingi dawa za kuingiza kwenye uke (vaginal pessaries) hutumika kwa muda wa siku 3 mpaka 6. Wakati mwingine dawa za kunywa zinaweza kutumika kutibu fangasi
Cotrimazole na fluconazole ni kati ya dawa zinazotumika mara kwa mara lakini pia pamoja na matibabu kuna hatari ya maambukizi ya fangasi hawa kujirudia kwakuwa Dawa zetu hizi zimekua zikitibu dalili na si chanzo cha tatizo hivyo ni muhimu kupata tiba mbadala na Ushauri zaidi  unapoona inajirudia

 pamoja na hayo ugonjwa huu unaweza kujikinga nao kwa kuepuka mambo mbalimbali na kufanya mambo yatakayotusaidia kutopata ugonjwa huu kwa kuzingatia kanuni ya afya na USAFI
👉Vaa chupi ambazo hazibani na zilizotengenezwa kwa pamba au hariri epuka kutumia chupi aina ya synthetic underwear
👉epuka kufanya mapenzi na mpenzi wako mwenye maambukizi haya hivyo ni vyema wapenzi wote wawili mkapata matibabu ya fangasi na mjitahidi kuwa waaminifu
👉kula mlo wenye virutubsho muhimu
👉epuka kuoga maji ya moto sana (Hot baths) tumia maji ya uvuguvugu
👉osha sehemu zako za siri kwa kutumia maji Safi na jikaushe kwa kutumia taulo au kitambaa Safi
👉epuka mavazi yote ya kubana ukeni
👉tumia ped na pantiliner zenye anions zenye uwezo wa kufyonza haraka (NEPLILY)
👉kunywa maziwa aina ya mtindi yenye live culture Mara kwa Mara yatakusaidia kuepusha maambukizi ya fangasi ukeni
👉epuka matumizi ya vifaa vya kupanga uzazi na vifaa vya kufanyia mapenzi (sex toys, diaphragm cervical caps) husababisha maambukizi ya fangasi ukeni
👉 epuka kutumia sabuni za kemikali

FAHAMU PEDI BORA ZA NEPLILY
ped za neplily zimetengenezwa kwa technologia ya hali ya juu,neplily pads na pantliner zimetengenezwa kwa anion chip technology,
Anion ni negative particles ambazo zinatoa oxygen pale zinapogusana na mwili wako,
Joto la mwili linapokutana na pedi au pantliner inaachia negative particles ambazo mwisho wa siku inatoa hewa safi ya oxygen.
anions hizi zinapatikana kwenye maporomoko ya maji,chemichemi ya maji kwenye misitu,mvua za acidi,moshi wa misitu baada ya kuunguzwa n.k.
faida za anion chip

1.inauwezo wa kuondoa muwasho,bacteria,fungus wa aina yoyote kipindi cha hedhi
2.inaondoa harufu mbaya
3.inarekebisha mzunguko na kuweka homoni sawa.
4.inapunguza uwezekano wa kupata ugumba
5.inaondoa msongo wa mawazo na uchovu kipindi cha Hedhi
6.inarekebisha mfumo wa homoni za mwili
7.pantliners pia zinatumika na wanaume wenye prostatic hypertrophy, bawa siri na kutokwa na damu kwenye njia ya haja kubwa
8.inauwezo wa kuondoa uvimbe na kuzibua mirija ya uzazi iliyoziba.
9.inaimarisha kinga ya mwili na kujikinga na matatizo yote ya uzazi.
10.inaondoa matatizo yote ya uzazi hasa baada ya kuogelea kwenye mabwawa ya kuogelea.
10.inatibu uti.
kwa ujumla neplily pads na pantiliner zina uwezo mkubwa wa kutokomeza matatizo yote yanayowakumba wanawake wakiwa kwenye siku zao.kama kuumwa kichwa,msongo wa mawazo,kuchoka,kuumwa tumbo,kuwa na flow kubwa na mengine mengi
ZITUMIENI ZITAWASAIDIA

NOTED :NDUGU MSOMAJI KAMA UNA MAONI/USHAUR NA UNASUMBULIWA NA TATIZO HILI WASILIANA NAMI NIANDIKIE UJUMBE KUPITIA NAMBA NA EMAIL HAPO CHINI

Makala hii imeandikwa na Dr Naytham S Masoud
nsalum998@gmail.com
+255623026602/+255746465095

KUPATA MAKALA ZAIDI ZA AFYA WAWEZA TEMBELEA BLOG HII naythamhealthcare.blogspot.com

naimain umejifunza Nami nashukuru kwa wew kujifunza hivyo nakuomba nawe uwafikishie elimu hii wengine KWA KUSHARE, KUKOMENT NA KUWAALIKA WENZAKO WALIKE PAGE HII

TATIZO LA UVIMBE KATIKA MAYAI (OVARIAN CYST)

FAHAMU ATHARI ZA UVIMBE KATIKA MAYAI YA MWANAMKE (OVARIAN CYST)

Asalaam alaykum warhmatullah wabarakatull,
 Naam natumaini mnaendelea vizuri napenda kumshukuru Mungu kwa kunijaalia Afya kuweza kuandika makala hii inayohusu uvimbe katika mayai ya mwanamke hivyo ungana nami rafiki kupata elimu hii

OVARIAN CYST NI NINI??
~Ni uvimbe unaotokea katika mayai ya mwanamke (ovarian)
~uvimbe huo hutokana na mkusanyiko wa maji maji yanayozungukwa na kutu nyembamba ndani ya mayai ya mwanamke
~uvimbe huu hutokea kwa wanawake wa rika tofauti na mara nyingi huonekana kwa wanawake waliofika umri wa kushika ujauzito
~uvimbe huu huweza kuwa na ukubwa wa cm3_cm30 na unaweza kujaza tumbo lote

AINA ZA UVIMBE KATIKA MAYAI YA MWANAMKE
(@)HEMORRHAGIC CYST ~hii ni Aina ya uvimbe ambayo hutokea wakati kukiwa na uvujaji wa damu ndani ya uvimbe wa Aina yoyote ule ambao umeshajitengeza tayari,pia uvimbe huu huambatana na maumivu makali kwenye upande mmoja wa ubavu (kushoto /kulia)

(@)FOLLICULAR CYST ~hii ni Aina ya uvimbe unaotokea wakati ovulation isipotokea au baada ya corpus luteum kuanza kusinyaa na kupotea yenyewe baada ya kutopachikwa kwa yai kwenye kuta za mfuko wa kizazi, pia uvimbe huu una ukubwa wa wastani 2:3 kwa upana, uvimbe huu hauna dalili yoyote na hupotea yenyewe baada ya Muda

(@)CORPUS LUTEUM ~hii ni Aina ya uvimbe ambazo unatokana na kutopachikwa kwa yai la uzazi lililorutubishwa na mbegu ya kiume kwenye mfuko wa kizazi, pia uvimbe huu husinyaa na kupotea wenyewe ingawa wakati mwingine huweza kujaa maji na kusababisha tumbo kuvimba upande mmoja

(@)DERMOID CYST ~uvimbe huu hujulikana kama MATURE CYST TERATOMA, huathiri wanawake wadogo walio katika umri wa kushika ujauzito na uvimbe huu huweza kukua nchi 6 kwa upana na ndani Yake huweza kuwa na mchanganyiko wa nywele, mifupa, mafuta na cartilage, pia uvimbe huu huweza kuwa mkubwa zaidi na kujizungusha hivyo huathiri mzunguko wa damu na hivyo kusababisha maumivu makali ya nyonga na tumbo.

(@)POLYCYSITIC APPEARING CYST ~huu ni uvimbe mkubwa sana na huwa umezungukwa na vijiuvimbe vidogo vidogo na huonekana hata kwa wanawake wenye Afya njema na wale wenye tatizo la homorne

(@)CYSTEDENOMA ~hii ni Aina ya uvimbe ambayo hutokea kwenye tissue za ovary na hujazwa na maji maji Aina ya kamasi pia uvimbe huu una ukubwa wa nch, 12 au zaidi kwa upana

(@)ENDOMETRIOSIS ~huu ni uvimbe unaosababishwa na uwepo wa Aina mojawapo ya kuta za mfuko wa kizazi unaojulikana kama ENDOMETRIUM kwenye mayai ya mwanamke, uvimbe huu huathiri wanawake walio katika umri wa kushika ujauzito na huambatana na maumivu makali (sugu) ya nyonga (CHRONIC PELVIC PAIN) wakati wa hedhi, pia uvimbe huu una rangi nyekundu ya kahawia (reddish brown) na una ukubwa wa 0.75_8 inches


VIHATARISHI VYA TATIZO HILI
👉kuwa na mzunguko wa hedhi usioeleweka (IRREGULAR MENSTRUATION CYCLE)
👉kuwa na mafuta mengi tumboni
👉kukosekana kwa uwiano wa vichocheo mwilini (hormone imbalance)
👉kuvunja ungo mapema yani kuanzia miaka 11kushuka chini
👉kutumia dawa za kemikali maana zina side effects

DALILI NA VIASHIRIA VYA TATIZO HILI
👉mwanamke kupata maumivu /kichomi ambayo huwa hayana Muda maalumu huchoma ukeni, kiunoni, mgongoni, mapaja, NK
👉kuhisi tumbo kuwa zito limejaa au kuvimba
👉kupata maumivu makali katika matiti
👉kutopata hedhi katika mpangilio
👉kuongezeka uzito mara kwa mara
👉kupata maumivu katika mbavu
👉kuumwa kichwa mara kwa mara
👉nywele kukua haraka kila wakati
👉kupata maumivu makali wakati wa hedhi
👉kuhisi kichefchef (kutapika)
👉kupata maumivu makali ya nyonga
👉kuhisi uchovu
Kila wakati
👉kutokwa na matone ya damu
👉kutoshika mimba
👉mabadiliko katika upatikanaji wa haja
@haja ndogo kutoka Bila kujielewa
(b) haja kubwa kuwa ngumu

VIPIMO NA MATIBABU
Matibabu hufanyika kwa kuangalia Majibu yaliyopatikana katika vipimo, Kuna vipimo vingi vya kuona tatizo hili kama vile ENDOVAGINAL ULTRA SOUND, COMPLETE BLOOD COULD, SERUM CA 125 ASSAY, URINE FOR PREGNANCY, baada ya daktar kupata Majibu ndio huangalia tiba inayoendana na Majibu yaliyopatikana katika vipimo mbalimbali, matibabu hayo huweza kuwa ya Aina mbili

(@)MATIBABU YA DAWA
~tiba hii huhusisha matumizi ya dawa za upangaji uzazi kwa Muda wa wiki 4_6, matumizi ya dawa Hizi kwa Muda mrefu huzuia kutokea tena uvimbe katika kizazi kwasababu dawa Hizi hufanya Kazi ya kuzuia mayai kutotoa mayai ya uzazi (ovums) pia dawa Hizi hazipunguzi uvimbe uvimbe kwasababu uvimbe utapotea wenyewe baada ya Muda

(B) TIBA YA UPASUAJI
~katika tiba hii ya upasuaji Kuna Aina mbili

(1)EXPLORATORY LAPARATOMY
~katika tiba hii mgonjwa hupasuliwa tumboni na daktar huweza kuondoa uvimbe, upasuaji huu hufanyika kwa mwanamke mwenye uvimbe ambao hauwezi kupotea na mkubwa kuanzia 5cm_10cm

(2)LAPARASCOPIC SURGERY
~huu ni upasuaji ambao daktari hupasua sehem ndogo na kutumbukiza mpira maalumu ambao una kamera kwa mbele na huondoa uvimbe katika mayai, upasuaji huu hupendwa na wanawake wengi kwasababu hauachi kovu lolote na mara nyingi hufanyika kwa uvimbe mmoja
NOTED :NDUGU RAFIKI hakikisha unaenda kupima Afya yako mara nyingi kwani Kuna watu wapo na tatizo hili ila wanashindwa kuelewa au hawajitambui hivyo ni bora ukaepuka ugonjwa huu kwani madhara Yake ni kusababisha UGUMBA.
Asante kwa kuwa nami kupata elimu hii rafiki kama una maswali, maoni, mapendekezo yoyote niandikie kupitia email  na namba yangu hapo chini

KUSOMA MAKALA MBALIMBALI ZA AFYA TEMBELEA KATIKA BLOG HII NAYTHAMHEALTHCARE.BLOGSPOT.COM

Makala hii imeandaliwa na Dr Naytham S Masoud
email:nsalum998@gmail.com
+255623026602/+255746465095
PLZ USISAHAU KUSHARE, KUKOMENT, KULIKE NA WATAG RAFIKI ZAKO