BREAKING
  • FANGASI UKENI

    Pata suluhisho la tatizo la fangasi ukeni pamoja na ushauri utakaokufanya uwe salama daima

  • TIBA YA NGUVU ZA KIUME

    Okoa nyumba yako kwa kupata dawa itakayo ongeza nguvu zako za kiume na kudumisha unyumba daima

  • SULUHISHO LA U.T.I

    Je hauna ufahamu wowote kuhusu U.T.I ?Je Unakabiliwa na tatizo la U.T.I?Wasiliana nami nikujuze zaidi huenda una tatizo la U.T.I lakini haujijui,na kama unalo basi tiba yake ipo

  • TIBA YA VIDONDA VYA TUMBO

    Je Umesumbuliwa na vidonda vya tumbo kwa muda mrefu pasina kupata suluhisho,wasiliana nami nikupatie dawa itakayoondoa tatizo lako kabisa

BannerFans.com

Alhamisi, 17 Novemba 2016

UGONJWA WA FANGAS UKENI (VAGINAL CANDIDIASIS)

FAHAM NAMNA YA KUJITIBU NA KUJILINDA DHIDI YA UGONJWA WA FANGASI UKENI (VAGINAL CANDIDIASIS)

Asalaam alaykum warhmatullah wabarakatul ndugu msomaji wa page hii,kutokana na kupokea maoni na maswali yenu leo nimependa kuzungumzia ugonjwa wa fangasi ukeni ambao ni common hususani kwa wanawake,

Maambukizi ya fangasi sehemu za siri imekua ni tatizo kubwa sana Duniani 75%ya wanawake wote Duniani wanasumbuliwa na tatizo hili,na maambukizi haya ya fangasi  husababishwa na fangasi aina ya CANDIDA ALBICANS lakini pia maambukizi haya hujulikana kama YEAST INFECTIONS /THRUSH

CANDIDA ALBICANS hupatikana katika midomo, mpira wa kupitishia Chakula (PHARYNX), kibofu cha mkojo, uume au katika uke
bacteria Hawa huishi katika sehemu hizo Bila kuleta madhara, isipokua pale mazingira ya eneo husika, yanapobadilika, MFANO mabadiliko katika Hali ya PH
tutambue PH ya mwanamke ndani ya uke ni 4.0_4.5 au uwiano wake na vimelea (microorganisms) wengine, hivyo huharibiwa kutokana na sababu mbalimbali kama vile MATUMIZI YA MADAWA YA ANTIBIOTICS eg AMPICILLINE, CIPROFLAXINE, AMOXYLINE, DOXYCYCLINE, ERTHROMYCINE, NK pia kupungua kwa Kinga kutokana na magonjwa mbalmbal nk

maambukizi ya fangasi ukeni yamegawanyika katika sehemu KUU mbili nazo ni ÷
(1)MAAMBUKIZI YASIYO MAKALI (UNCOMPLICATED THRUSH)
~katika aina hii mgonjwa hupatwa na maambukizi Mara moja hadi nne kwa mwaka pia Dalili zake huwa si za kuogopesha na maambukizi haya husababishwa na fangasi aina ya CANDIDA ALBICANS

(2)MAAMBUKIZI MAKALI (COMPLICATED THRUSH)
Katika kundi hili mgonjwa hupatwa na maambukizi Zaidi ya Mara nne au Zaidi kwa mwaka pia Dalili zake huwa ni za kuogopesha kama maambukizi yatakua yametokea kipindi cha UJAUZITO, ugonjwa wa VVU, ugonjwa wa sukari nk

VIHATARISHI VYA MAAMBUKIZI YA FANGASI KATIKA UKE
~Mabadiliko ya mfumo wa homoni mwilini ambazo husababisha mabadiliko katika sehemu za siri
~magonjwa ya saratani ya tezi koo la Chakula (thyroid cancer)
~wanawake wenye umri wa miaka 20_30 wapo katika hatari ya kupata maambukizi haya wakati wale ambao wameshaacha kupata hedhi (menopause) na wale ambao hawajaanza kupata hedhi hawako katika hatari kutokana na mazingira na vitu wanavyotumia
~upungufu wa Kinga mwilin kutokana na magonjwa hatar ya saratani, kisukari, ugonjwa wa mononucleosis nk
~matumizi ya vidonge vya majira
~msongo wa mawazo
~kujamiana kwa njia ya kawaida Mara tu baada ya kujamiiana kupitia haja kubwa (anal sex)
~matumizi ya glycerin wakati wa kujamiiana husababisha maambukizi pia
~kuwa na historia ya kupata matibabu ya homoni (hormonal replacement therapy)
~ujauzto (husababisha kubadilika kwa mfumo wa homoni mwilini
~kuwa na utapiamlo (malnutrition
~kuvaa nguo za ndani ziszo kauka vzur
~kuvaa mavazi yanayoleta sana joto sehem za siri

DALILI ZA UGONJWA WA FANGASI UKENI
👉kuwashwa sehem za siri
👉kuhisi maumivu makali wakati wa kujamiiana (superficial dysapareunia)
👉kuhisi kuwaka moto sehemu za siri Mara baada ya kutoka kufanya tendo la ndoa au kutoka kukojoa (burning sensation
👉kupata vidonda ukeni (soreness
👉kuvimba na kuwa mwekundu katika mdomo wa nnje wa uke (labia minora
👉kupata maumivu wakati wa kukojoa
👉kutokwa na uchafu wa rangi nyeupe au kijivu unaoweza kuwa MWEPESI au MZITO au majimaji
NOTED :Dalili na viashiria hivi huwa mbaya Zaidi mwanamke anapokua mwezini

MATIBABU NA JINSI YA KUJIKINGA NA UGONJWA HUU WA FANGASI UKENI
Matibabu ya fangasi ya uke hutumia dawa za kuua fangasi (antifungals).  Mara nyingi dawa za kuingiza kwenye uke (vaginal pessaries) hutumika kwa muda wa siku 3 mpaka 6. Wakati mwingine dawa za kunywa zinaweza kutumika kutibu fangasi
Cotrimazole na fluconazole ni kati ya dawa zinazotumika mara kwa mara lakini pia pamoja na matibabu kuna hatari ya maambukizi ya fangasi hawa kujirudia kwakuwa Dawa zetu hizi zimekua zikitibu dalili na si chanzo cha tatizo hivyo ni muhimu kupata tiba mbadala na Ushauri zaidi  unapoona inajirudia

 pamoja na hayo ugonjwa huu unaweza kujikinga nao kwa kuepuka mambo mbalimbali na kufanya mambo yatakayotusaidia kutopata ugonjwa huu kwa kuzingatia kanuni ya afya na USAFI
👉Vaa chupi ambazo hazibani na zilizotengenezwa kwa pamba au hariri epuka kutumia chupi aina ya synthetic underwear
👉epuka kufanya mapenzi na mpenzi wako mwenye maambukizi haya hivyo ni vyema wapenzi wote wawili mkapata matibabu ya fangasi na mjitahidi kuwa waaminifu
👉kula mlo wenye virutubsho muhimu
👉epuka kuoga maji ya moto sana (Hot baths) tumia maji ya uvuguvugu
👉osha sehemu zako za siri kwa kutumia maji Safi na jikaushe kwa kutumia taulo au kitambaa Safi
👉epuka mavazi yote ya kubana ukeni
👉tumia ped na pantiliner zenye anions zenye uwezo wa kufyonza haraka (NEPLILY)
👉kunywa maziwa aina ya mtindi yenye live culture Mara kwa Mara yatakusaidia kuepusha maambukizi ya fangasi ukeni
👉epuka matumizi ya vifaa vya kupanga uzazi na vifaa vya kufanyia mapenzi (sex toys, diaphragm cervical caps) husababisha maambukizi ya fangasi ukeni
👉 epuka kutumia sabuni za kemikali

FAHAMU PEDI BORA ZA NEPLILY
ped za neplily zimetengenezwa kwa technologia ya hali ya juu,neplily pads na pantliner zimetengenezwa kwa anion chip technology,
Anion ni negative particles ambazo zinatoa oxygen pale zinapogusana na mwili wako,
Joto la mwili linapokutana na pedi au pantliner inaachia negative particles ambazo mwisho wa siku inatoa hewa safi ya oxygen.
anions hizi zinapatikana kwenye maporomoko ya maji,chemichemi ya maji kwenye misitu,mvua za acidi,moshi wa misitu baada ya kuunguzwa n.k.
faida za anion chip

1.inauwezo wa kuondoa muwasho,bacteria,fungus wa aina yoyote kipindi cha hedhi
2.inaondoa harufu mbaya
3.inarekebisha mzunguko na kuweka homoni sawa.
4.inapunguza uwezekano wa kupata ugumba
5.inaondoa msongo wa mawazo na uchovu kipindi cha Hedhi
6.inarekebisha mfumo wa homoni za mwili
7.pantliners pia zinatumika na wanaume wenye prostatic hypertrophy, bawa siri na kutokwa na damu kwenye njia ya haja kubwa
8.inauwezo wa kuondoa uvimbe na kuzibua mirija ya uzazi iliyoziba.
9.inaimarisha kinga ya mwili na kujikinga na matatizo yote ya uzazi.
10.inaondoa matatizo yote ya uzazi hasa baada ya kuogelea kwenye mabwawa ya kuogelea.
10.inatibu uti.
kwa ujumla neplily pads na pantiliner zina uwezo mkubwa wa kutokomeza matatizo yote yanayowakumba wanawake wakiwa kwenye siku zao.kama kuumwa kichwa,msongo wa mawazo,kuchoka,kuumwa tumbo,kuwa na flow kubwa na mengine mengi
ZITUMIENI ZITAWASAIDIA

NOTED :NDUGU MSOMAJI KAMA UNA MAONI/USHAUR NA UNASUMBULIWA NA TATIZO HILI WASILIANA NAMI NIANDIKIE UJUMBE KUPITIA NAMBA NA EMAIL HAPO CHINI

Makala hii imeandikwa na Dr Naytham S Masoud
nsalum998@gmail.com
+255623026602/+255746465095

KUPATA MAKALA ZAIDI ZA AFYA WAWEZA TEMBELEA BLOG HII naythamhealthcare.blogspot.com

naimain umejifunza Nami nashukuru kwa wew kujifunza hivyo nakuomba nawe uwafikishie elimu hii wengine KWA KUSHARE, KUKOMENT NA KUWAALIKA WENZAKO WALIKE PAGE HII

TATIZO LA UVIMBE KATIKA MAYAI (OVARIAN CYST)

FAHAMU ATHARI ZA UVIMBE KATIKA MAYAI YA MWANAMKE (OVARIAN CYST)

Asalaam alaykum warhmatullah wabarakatull,
 Naam natumaini mnaendelea vizuri napenda kumshukuru Mungu kwa kunijaalia Afya kuweza kuandika makala hii inayohusu uvimbe katika mayai ya mwanamke hivyo ungana nami rafiki kupata elimu hii

OVARIAN CYST NI NINI??
~Ni uvimbe unaotokea katika mayai ya mwanamke (ovarian)
~uvimbe huo hutokana na mkusanyiko wa maji maji yanayozungukwa na kutu nyembamba ndani ya mayai ya mwanamke
~uvimbe huu hutokea kwa wanawake wa rika tofauti na mara nyingi huonekana kwa wanawake waliofika umri wa kushika ujauzito
~uvimbe huu huweza kuwa na ukubwa wa cm3_cm30 na unaweza kujaza tumbo lote

AINA ZA UVIMBE KATIKA MAYAI YA MWANAMKE
(@)HEMORRHAGIC CYST ~hii ni Aina ya uvimbe ambayo hutokea wakati kukiwa na uvujaji wa damu ndani ya uvimbe wa Aina yoyote ule ambao umeshajitengeza tayari,pia uvimbe huu huambatana na maumivu makali kwenye upande mmoja wa ubavu (kushoto /kulia)

(@)FOLLICULAR CYST ~hii ni Aina ya uvimbe unaotokea wakati ovulation isipotokea au baada ya corpus luteum kuanza kusinyaa na kupotea yenyewe baada ya kutopachikwa kwa yai kwenye kuta za mfuko wa kizazi, pia uvimbe huu una ukubwa wa wastani 2:3 kwa upana, uvimbe huu hauna dalili yoyote na hupotea yenyewe baada ya Muda

(@)CORPUS LUTEUM ~hii ni Aina ya uvimbe ambazo unatokana na kutopachikwa kwa yai la uzazi lililorutubishwa na mbegu ya kiume kwenye mfuko wa kizazi, pia uvimbe huu husinyaa na kupotea wenyewe ingawa wakati mwingine huweza kujaa maji na kusababisha tumbo kuvimba upande mmoja

(@)DERMOID CYST ~uvimbe huu hujulikana kama MATURE CYST TERATOMA, huathiri wanawake wadogo walio katika umri wa kushika ujauzito na uvimbe huu huweza kukua nchi 6 kwa upana na ndani Yake huweza kuwa na mchanganyiko wa nywele, mifupa, mafuta na cartilage, pia uvimbe huu huweza kuwa mkubwa zaidi na kujizungusha hivyo huathiri mzunguko wa damu na hivyo kusababisha maumivu makali ya nyonga na tumbo.

(@)POLYCYSITIC APPEARING CYST ~huu ni uvimbe mkubwa sana na huwa umezungukwa na vijiuvimbe vidogo vidogo na huonekana hata kwa wanawake wenye Afya njema na wale wenye tatizo la homorne

(@)CYSTEDENOMA ~hii ni Aina ya uvimbe ambayo hutokea kwenye tissue za ovary na hujazwa na maji maji Aina ya kamasi pia uvimbe huu una ukubwa wa nch, 12 au zaidi kwa upana

(@)ENDOMETRIOSIS ~huu ni uvimbe unaosababishwa na uwepo wa Aina mojawapo ya kuta za mfuko wa kizazi unaojulikana kama ENDOMETRIUM kwenye mayai ya mwanamke, uvimbe huu huathiri wanawake walio katika umri wa kushika ujauzito na huambatana na maumivu makali (sugu) ya nyonga (CHRONIC PELVIC PAIN) wakati wa hedhi, pia uvimbe huu una rangi nyekundu ya kahawia (reddish brown) na una ukubwa wa 0.75_8 inches


VIHATARISHI VYA TATIZO HILI
👉kuwa na mzunguko wa hedhi usioeleweka (IRREGULAR MENSTRUATION CYCLE)
👉kuwa na mafuta mengi tumboni
👉kukosekana kwa uwiano wa vichocheo mwilini (hormone imbalance)
👉kuvunja ungo mapema yani kuanzia miaka 11kushuka chini
👉kutumia dawa za kemikali maana zina side effects

DALILI NA VIASHIRIA VYA TATIZO HILI
👉mwanamke kupata maumivu /kichomi ambayo huwa hayana Muda maalumu huchoma ukeni, kiunoni, mgongoni, mapaja, NK
👉kuhisi tumbo kuwa zito limejaa au kuvimba
👉kupata maumivu makali katika matiti
👉kutopata hedhi katika mpangilio
👉kuongezeka uzito mara kwa mara
👉kupata maumivu katika mbavu
👉kuumwa kichwa mara kwa mara
👉nywele kukua haraka kila wakati
👉kupata maumivu makali wakati wa hedhi
👉kuhisi kichefchef (kutapika)
👉kupata maumivu makali ya nyonga
👉kuhisi uchovu
Kila wakati
👉kutokwa na matone ya damu
👉kutoshika mimba
👉mabadiliko katika upatikanaji wa haja
@haja ndogo kutoka Bila kujielewa
(b) haja kubwa kuwa ngumu

VIPIMO NA MATIBABU
Matibabu hufanyika kwa kuangalia Majibu yaliyopatikana katika vipimo, Kuna vipimo vingi vya kuona tatizo hili kama vile ENDOVAGINAL ULTRA SOUND, COMPLETE BLOOD COULD, SERUM CA 125 ASSAY, URINE FOR PREGNANCY, baada ya daktar kupata Majibu ndio huangalia tiba inayoendana na Majibu yaliyopatikana katika vipimo mbalimbali, matibabu hayo huweza kuwa ya Aina mbili

(@)MATIBABU YA DAWA
~tiba hii huhusisha matumizi ya dawa za upangaji uzazi kwa Muda wa wiki 4_6, matumizi ya dawa Hizi kwa Muda mrefu huzuia kutokea tena uvimbe katika kizazi kwasababu dawa Hizi hufanya Kazi ya kuzuia mayai kutotoa mayai ya uzazi (ovums) pia dawa Hizi hazipunguzi uvimbe uvimbe kwasababu uvimbe utapotea wenyewe baada ya Muda

(B) TIBA YA UPASUAJI
~katika tiba hii ya upasuaji Kuna Aina mbili

(1)EXPLORATORY LAPARATOMY
~katika tiba hii mgonjwa hupasuliwa tumboni na daktar huweza kuondoa uvimbe, upasuaji huu hufanyika kwa mwanamke mwenye uvimbe ambao hauwezi kupotea na mkubwa kuanzia 5cm_10cm

(2)LAPARASCOPIC SURGERY
~huu ni upasuaji ambao daktari hupasua sehem ndogo na kutumbukiza mpira maalumu ambao una kamera kwa mbele na huondoa uvimbe katika mayai, upasuaji huu hupendwa na wanawake wengi kwasababu hauachi kovu lolote na mara nyingi hufanyika kwa uvimbe mmoja
NOTED :NDUGU RAFIKI hakikisha unaenda kupima Afya yako mara nyingi kwani Kuna watu wapo na tatizo hili ila wanashindwa kuelewa au hawajitambui hivyo ni bora ukaepuka ugonjwa huu kwani madhara Yake ni kusababisha UGUMBA.
Asante kwa kuwa nami kupata elimu hii rafiki kama una maswali, maoni, mapendekezo yoyote niandikie kupitia email  na namba yangu hapo chini

KUSOMA MAKALA MBALIMBALI ZA AFYA TEMBELEA KATIKA BLOG HII NAYTHAMHEALTHCARE.BLOGSPOT.COM

Makala hii imeandaliwa na Dr Naytham S Masoud
email:nsalum998@gmail.com
+255623026602/+255746465095
PLZ USISAHAU KUSHARE, KUKOMENT, KULIKE NA WATAG RAFIKI ZAKO

TATIZO LA KUVIMBA KWA KIZAZI CHA MWANAMKE (ADENOMYOSIS)

FAHAMU TATIZO LA KUVIMBA KWA KIZAZI CHA MWANAMKE (ADENOMYOSIS) LINAVYOWAANGAMIZA NA KUWAKOSESHA RAHA WANAWAKE

Asalam alaykum warhmatullah wabarakatul mpenzi msomaji wa makala hii natumaini unaendelea vizuri na majukumu ya kila siku, namshukuru Mungu kuniwezesha leo tena kuandika makala ili kukuwezesha ndugu msomaji kufahamu mambo mengi kuhusu Afya ya mwanamke na mzunguko mzuri wa hedhi, leo napenda kuzungumzia tatizo la kuvimba kwa kizazi cha mwanamke ambapo kitaalamu tunasema ni ADENOMYOSIS pia tatizo hili kwa zamani lilijulikana kama ENDOMETRIOSIS INTERNA

ADENOMYOSIS NI NINI?
~Ni tatizo ambalo nyama hutokea na kukua kama tabaka au ukuta mwingine juu ya misuli ya kizazi(ectopic glandular tissues)
~tatizo hili huwaathiri zaidi wanawake walio kati ya miaka 35_50, ingawa katika Hali isiyo ya kawaida hutokea katika umri wa chini ya miaka 35
~tatizo hili la kuvimba kwa kizazi linapotokea huambatana na damu nyingi wakati wa hedhi na kupata maumivu makali wakati wa hedhi pia maumivu huongezeka zaidi pale tabaka la ndani ya kizazi linapojikita katikati ya misuli ya kizazi na hivyo mwanamke mwenye tatizo hili la kuvimba kwa kizazi hupata maumivu makali chini ya tumbo ktk kitovu Muda wote pasipo kupata damu ya hedhi hata kama tarehe za kupata damu (period) zimefikia, pia damu huweza kutoka kwa wingi pia kizazi huendelea kuvimba kutokana na tabaka la ndani (basal endometrium) kujipenyeza ndani ya misuli ya kizazi na hivyo kusababisha kila siku kizazi kuendelea kukua na mwanamke kuonekana kama ana ujauzito na tumbo huwa gumu hata hivyo tatizo hili ni tofauti na tatizo la uvimbe katika kizazi (fibroids)

CHANZO CHA TATIZO HILI LA KUVIMBA KWA KIZAZI
~Chanzo halisi cha tatizo hili bado hakijafanikiwa kuwa wazi ingawa misuli ya kizazi (uterine trauma) huchangia hili kwa kuwa huondoa ukingo wa tabaka la ndani ya kizazi kuelekea katika misuli ya kizazi pia utoaji wa mimba hovyo husababisha mirija kuchubuka pia matokeo mabaya ya uwekaji wa lupu

DALILI ZA TATIZO HILI
Dalili au viashiria vya tatizo hili ni vingi ila hata hivyo Kuna baadhi ya wanawake wenye tatizo hili hawaonyeshi dalili yoyote huku kizazi kikizid kuvimba na wengine huhisi maumivu makali ya kizazi Muda wote au wakati wa hedhi
Dalili zenyewe ni Hizi
👉chembechembe za tabaka la ndani ya kizazi linapojikita katikati ya misuli ya kizazi huendelea kutoa damu hivyo kusababisha damu kuvujia ndani kwa ndani Bila damu hiyo kutoka nnje
👉mwanamke huhisi uchungu wa uzazi na kuhisi kama vile anataka kujifungua kwa kuwa hupata shinikizo ukeni
👉mwanamke huhisi maumivu makali chini ya tumbo Muda wote na kila akienda katika hospital hukutwa ana uti kitu ambacho sio kweli
👉mwanamke huhisi maumivu makali zaidi kipindi cha upevushaji mayai (ovulation) au kipindi cha period (hedhi)
👉mwanamke huhisi mkojo kila wakati kutokana na kibofu kugandamizwa na shinikizo la kizazi
👉mwanamke hutoka damu kupita kiasi hadi pedi huwa hazitoshelezi pia wakati wa hedhi tumbo hubana au kukaza (abdominal eramps) Muda wote na mwanamke hutamani kuinama tu

MATIBABU NA VIPIMO
matibabu ya tatizo hili hufanyika katika kliniki Za akina mama kwenye hospital za mkoa, private na daktar hutibu kutokana na Majibu yaliyopatikana katika vipimo vya MRI, ULTRASOUND na matibabu hayo huweza kuwa ya dawa za HOMONI kutegemea na ukubwa wa tatizo pia tiba nyingine ni upasuaji hasa wa kuondoa kizazi kitu ambacho hugharim sana maisha ya mahusiano iwapo mhusika hakuzaa na pia endapo mwanamke atapata tatizo hili akiwa mjamzito basi mimba Yake hutoka na hupata uchungu mapema kabla ya siku ya kujifungua

USHAURI :WANAWAKE WENGI HUWA NA DESTURI YA KUPUUZA KWENDA HOSPTAL KWA KUONA TATIZO NI DOGO HVYO NDUGU RAFIKI HAKIKISHA UNAENDA KUPIMA AFYA YAKO MARA KWA MARA ILI KUWEZA KUTAMBUA MATATIZO MAPEMA HIVYO TUACHE TABIA YA KUPUUZIA KITU HATA KAMA NI KIDOGO
Asante kwa kuwa nami kupata elimu hii rafiki kama una maswali/maoni au mapendekezo yoyote niandikie kupitia email na namba yangu hapo chini

KUSOMA ZAIDI MAKALA ZA AFYA TEMBELEA BLOG HII
naythamhealthcare.blogspot.com

Makala hii imeandaliwa na Dr Naytham S Masoud
Email:nsalum998@gmail.com/+255623026602/+255746465095

PLZ USISAHAU KUSHARE, KUKOMENT, KULIKE NA WATAG RAFIKI ZAKO

MAAMBUKIZI KATIKA VIA VYA UZAZI/PID (PELVIC INFLAMMATORY DISEASE)

FAHAM UGONJWA WA PID (PELVIC INFLAMMATORY DISEASE AU MAAMBUKIZI KATIKA VIA VYA UZAZI)

Asalaam alaykum warhmatullah wabarakatul ndugu zangu ni matumaini yangu mnaendelea vyema kabisa,napenda kuwataka radhi na kuwapa pole Kwa ukimya wangu kutokana na kupisha shughuli za uchaguzi, Nimepokea emails zenu nyingi sana za kunimiss nimefarijika napenda kuwaambia nami NIMEWAMISS NA NINAWAPENDA WOTE pamoja na hayo nimeona emails zenu zinazohusu magonjwa mbalimbali yanayowasumbua wanawake wengi na hivyo Leo hii napenda nianze na ugonjwa wa PID(PELVIC INFLAMMATORY DISEASE AU MAAMBUKIZI KATIKA VIA VYA UZAZI )

UGONJWA WA PID NI NINI??
~ni ugonjwa wa maambukizi unaotokea katika via vya uzazi wa mwanamke ambapo huhusisha maambukizi katika shingo ya kizazi (CERVICITIS),nyama katika mfuko wa uzazi (ENDOMETRITIS) na mirija ya uzazi (SALPINGITIS)

VYANZO NA VIHATARISHI VYA KUPATA UGONJWA WA PID (PELVIC INFLAMMATORY DISEASE)
Vimelea aina ya NEISSERIA GONORHOEAE pamoja na CHLAMYDIA TRACHOMATIS ndio chanzo cha maambukizi ya ugonjwa wa PID ingawaje kuna aina kadhaa za vimelea vinahusishwa kusababisha ugonjwa wa PID hivyo nilivyotaja ndio vinaongoza Kwa umaarufu kusababisha ugonjwa wa PID
~pamoja na vimelea hao kuwa chanzo kikuu cha ugonjwa wa PID zipo njia kadhaa hatarishi kusababisha maambukizi haya Nazo ni ÷
👉kutumia vipandikizi vya ndani ya mfuko wa uzazi(IUCD) kama njia mojawapo ya uzazi wa mpango
👉Kufanya ngono isiyo salama
👉Maambukizi ya njia za uzazi mara baada ya kujifungua au mimba kuharibika
👉Kuambukizwa kupitia damu yenye vimelea wa PID
👉Kupata maambukizi wakati wa kutoa mimba kwa njia isiyo salama

DALILI/VIASHIRIA VYA UGONJWA WA PID
Kuna dalili mbalimbali zinazoweza kuashiria ugonjwa huu wa PID miongoni mwa dalili hizo ni
👉Mwanamke kupata maumivu ya tumbo hasa maeneo ya chini ya kitovu
👉Kupata maumivu wakati wa kukojoa
👉Kupata homa na kuhisi kichefuchefu
👉Kupata maumivu ya mgongo na kutapika
👉Kutokwa na hedhi bila mpangilio
👉kupata maumivu wakati wa tendo la ndoa
👉Kutokwa na uchafu(utoko)mweupe ukeni unaotoa harufu mbaya

VIPIMO NA MATIBABU YA UGONJWA WA PID
Matibabu ya tatizo hili yanapatikana kote nchini kwa kufata misingi ya utabibu kuzingatia majibu yaliyopatikana katika vipimo mbalimbali ili kuweza kubaini tatizo kwa kufanya vipimo tofauti
MFANO
👉FULL BLOOD PICTURE _kipimo hiki kinatumika ili kuweza kutambua aina  mbalimbali za chembe damu zilizoathiriwa na maambukizi ya PID
👉CERVICAL CULTURE_Hutumika ili kujulia aina ya vimelea waliosababisha PID
👉ULTRASOUND _hutumika kuangalia katika nyonga kama kuna athari yoyote imetokea katika mfumo wa uzazi
~mara baada ya kufanya vipimo na mgonjwa kugundulika kama ameathirika na tatizo hili mara nyingi dawa za antibiotics ambazo ni DOXYCYCLINE,CEFOXITIN,MYCIN,GENTAMYCIN,CLINDAMYCIN,SULBACTAM,AMPICILLIN, huhusika kwa ajili ya kuua vimelea vya ugonjwa huu lakini ieleweke kuwa matumizi ya dawa hizi hufuata miongozo mbalimbali  ambayo imewekwa na mamlaka na wizara  ya afya kati ya sehem moja hadi nyingine hivyo si ruhusa kujinunulia dawa na kumeza pasipo ushauri wa daktari

NAMNA YA KUJIEPUSHA NA UGONJWA WA PID
Pamoja na kuwepo kwa dawa za kutibu tatizo hili ni vyema ukajiepusha na  vihatarishi vya kupata tatizo hili kwa kuzingatia yafuatayo
👉EPUKA KUFANYA NGONO ZEMBE
👉JIWEKEE TABIA YA KUFANYA VIPIMO MARA KWA MARA HASA KIZAZI
👉USIFANYE MAPENZI MARA BAADA YA KUJIFUNGUA AU MIMBA KUTOKA MPAKA UTAKAPOHAKIKISHA SHINGO YA UZAZI IMEFUNGA VEMA
👉KUWAHI KUONANA NA DAKTARI UNAPOONA DALILI ZA UGONJWA
👉KUWA MSAFI NA KULA LISHE BORA
NOTED:NDUGU RAFIKI UONAPO DALILI ZA UGONJWA HUU WAHI KUPATA MATIBABU KWANI UGONJWA HUU NI MKUBWA HUWEZA KUSABABISHA UGUMBA  IKIWA HAUTAPATA TIBA VIZURI

Kwa makala zaidi za afya tembelea blog yangu hapo chini
naythamhealthcare.blogspot.com

asante kwa kuwa nami kusoma ujumbe huu rafiki kama una MAONI/MASWALI NIANDIKIE KUPITIA NAMBA NA EMAIL YANGU HAPO CHINI PIA TAFADHALI NISAIDIE KUIFIKISHA ELIMU HII KWA WENGINE

Makala hii imeandaliwa na
Dr Naytham
+255623026602/+255746465095
email;nsalum998@gmail.com
naythamhealthcare.blogspot.com
USISAHAU KULIKE,KUKOMENT NA KUSHARE NA RAFIKI ZAKO

MZUNGUKO WA HEDHI NA MATATIZO YAKE

FAHAMU KUHUSU MZUNGUKO WA HEDHI NA MATATIZO YAKE (MENSTRUATION)

Asaalam alaykum warhmatullah wabarakatul  ndugu Rafiki uliyeamua kuungana Nami kufanikisha zoezi hili la kuwasaidia wakina mama na wasichana wengi kupata elimu ili waweze kudumisha afya yao na kupata mzunguko wa hedhi ulio salama, napenda kukushukuru na kukuomba uendelee kuwa Nami kuweza kuwasaidia wakina mama na mungu atatulipa kutokana na juhudi zetu kuwasaidia wenye uhitaji

NINI MAANA YA MZUNGUKO WA HEDHI???
Ni mzunguko wa kila mwezi ambao husababisha kutokwa kwa damu kila mwezi ukeni kutokana na mimba kutotungwa,
~mzunguko wa damu umegawanyika katika maeneo makuu mawili( 1)MZUNGUKO WA DAMU UNAOPEVUSHA MAYAI (OVULATORY CYCLE)
(2)MZUNGUKO WA DAMU USIOPEVUSHA MAYAI (ANOVULATORY CYCLE)

Napenda tufahamu kwa kina mizunguko hii
MZUNGUKO WA HEDHI UNAOPEVUSHA MAYAI (OVULATORY CYCLE) ~katika mzunguko huu mwanamke hutokwa na ute ute wa Uzazi ambao unavutika na katika mzunguko huu mtu anaweza kupata ujauzito

MZUNGUKO WA HEDHI USIOPEVUSHA MAYAI (ANOVULATORY CYCLE) ~katika mzunguko huu mwanamke hatoki ute ute wa Uzazi hivyo hawezi kupata ujauzito
~ pamoja na mizunguko hii miwili kutofautiana mwanamke hupata hedhi kama kawaida hata hivyo mwanamke ambaye mzunguko wake wa Hedhi  hapati ute ute wa Uzazi hawezi kupata ujauzito kutokana na mabadiliko ya mfumo wa homoni
 pia napenda mfaham kuwa ute ute wa Uzazi umegawanyika katika Makundi makuu matatu ambayo ni (1)UTE MWEPESI
(2)UTE UNAOVUTIKA
(3)UTE MZITO
Mara nyingi wanawake wasiopevusha mayai hawawezi kupata ujauzito hivyo huwa hawapati ute wa Uzazi na pia wengine hupata ute mzito daima kama uchafu unaotoka ukeni Lakini wenyewe hauna harufu wala muwasho

JINSI YA KUTAMBUA MZUNGUKO WAKO WA HEDHI
~Kila mwezi ovari za mwanamke huzalisha yai moja ambalo Lina uwezo wa kukaa kwa muda wa masaa 36 ndani ya mirija ya Uzazi hivyo inapotokea yai hili halijarutubishwa ukuta wa mji wa Uzazi hubomoka na kutoka nje ya uke pamoja na damu  kwa neno Moja tunasema siku za hedhi,
mzunguko wa hedhi huanza kuhesabiwa siku ya kwanza mwanamke anapoanza kupata siku zake,
Pia mzunguko wa hedhi uwe unaopevusha mayai au usiopevusha umegawanyika katika Makundi ya mizunguko mitatu yani MZUNGUKO MFUPI, MREFU NA WA KAWAIDA
~(1)MZUNGUKO MFUPI ~huu ni mzunguko wa siku 22_27
~(2)MZUNGUKO MREFU ~huu ni mzunguko wa siku 31_35
~(3)MZUNGUKO WA KAWAIDA ~huu ni mzunguko wa siku 28_30

JINSI YA KUSOMA MZUNGUKO WAKO
Tuchukulie mzunguko mfupi ambao ni siku 28
~siku ya kwanza mpaka ya tano huwa ni kipindi cha mwanamke kuingia katika mzunguko hivyo ni mwanzo wa mzunguko katika kipindi hiki ukuta wa mji wa mimba hubomoka na kutoka nnje pamoja na damu ukeni (siku ya hedhi) Katika kipindi hiki homoni za estrogen na progesterone huwa ndogo pia katika kipindi cha siku ya 6_10 ni kipindi ambacho ukuta wa Uzazi huanza kujengwa Tena kwa ajil ya kupokea kiini tete kipindi hiki mwanamke hawezi kupata mimba ila ni kipindi ambacho kinaelekea katika hatari hivyo katika kipindi hiki homoni za oestrogen huwa nyingi hivyo katika kipindi hiki yai huzalishwa (ovulation) siku ya kumi na moja ya mzunguko pia huweza kukaa kwa muda wa masaa 36 yani hutoka katika ovari na kusafiri katika mirija ya falopia mpaka siku ya kumi na nane na katika kipindi hiki homoni ya progesterone huzalishwa kwa wingi kwa ajili ya kutunza mji wa mimba pia homoni ya progesterone hupungua mwishoni mwa mzunguko yani kupungua huku husababisha mwanamke kuingia Tena katika mzunguko wa hedhi
~kipindi ambacho mwanamke ana breed hupata damu ya rangi nyekundu na huwa Ina mabonge kias kidogo na hutoka kiasi cha ML 35_50 kwa saa.
~kwa Kawaida ni kitu kizuri na cha kufurahia mwanamke kuona breed ila kutokana na matatizo wanayokutana nayo wanawake hujikuta wakichukia kuona siku zao kutokana na maumivu au adha mbalimbali wazipatazo. Ambazo ni
 (1)MAUMIVU MAKALI WAKATI WA HEDHI
(2)KUKOSA HEDHI AU KUPATA KATIKA MPANGILIO USIO SAHIHI
(3)KUTOKWA NA DAMU NYINGI
Leo tuanzie hili suala la maumivu makali wakati wa hedhi na namna ya kutatua
MAUMIVU MAKALI WAKATI WA HEDHI (DYSMENORHOEA)

Maumivu wakati wakati wa hedhi ni suala linalo wakumba wanawake wengi, takriban asilimia 15 ya wanawake wote duniani hupata maumivu haya wakati wa hedhi.
Maumivu haya huwa makali kiasi kwamba humunyima mwanamke uhuru wa kufanya kazi zake za kila siku.
Research zinaonesha kwa baadhi ya wanawake maumivu haya hupungua baada ya kujifungua na wengine huendelea kupata maumivu haya mpaka kikomo cha hedhi.

CHANZO CHA MAUMIVU WAKATI WA HEDHI
Chanzo kikuu cha tatizo hili ni UWINGI WA HOMONI YA KIKE (oestrogen ), homoni hii ndio inayohusika na mfumo mzima wa mzunguko wa hedhi na inapozidi hupelekea kuongezeka kwa fat cells katika cell membrane zilizoko kwenye ukuta wa mimba (uterus) hivyo kupelekea uzalishwaji mkubwa wa chemikali ziitwazo prostaglandins.

MADHARA YA HIZI PROSTAGLANDINS
siku chache kabla ya kupata hedhi, ukuta wa ndani wa mfuko wa kizazi hutengeneza prostaglandins kwa wingi na chemikali hizi huvunjika mwanamke anapokuwa period, chemikali hizi huleta mambo yafuatayo;
1. hupunguza ukubwa wa mishipa ya damu iliyo katika mfuko wa kizazi hivyoo kupelekea misuli ya maeneo hayo kukunjana na kukakamaa na hivyo kupelekea maumivu makali wakati wa hedhi.
2. Baadhi ya chemikali hizi huingia kwenye mfumo wa damu na kupelekea mwanamke kupata kichefuchefu, kichwa kuuma, kutapika na wakati mwingine kuharisha.

NJIA HIZI ZA KUFANYA UEPUKANE NA TATIZO HILI:

1.  Tumia vyakula vyenye mafuta kidogo.
unapotumia vyakula vyenye mafuta kidogo husaidia kupunguza kiwango cha cha mafuta kitumikacho kutengeneza chemikali hizi ziitwazo prostaglandins na hivyo kukufanya uepukane na maumivu haya wakati wa hedhi.

 VYAKULA VYENYE MAFUTA KIDOGO
vyakula vyote vitokanavyo na mimea (plant based diet )
huwa na kiwango kidogo cha mafuta ikilinganishwa na vyakula vitokanavyo na wanyama kwahiyo Anza leo kutumia vyakula vitokanavyo na mimea.
lakini pia wakati wa upishi wa chakula weka mafuta kidogo katika chakula chako kuzuia uwingi wa mafuta utakaochukuliwa na mwili.

2. Kula vyakula vyenye nyuzinyuzi (high fiber diet)
Vyakula hivi hutumika kupunguza na pia kubalance homoni ya kike kwani oestrogen inapotoka kwenye damu huchukuliwa na ini na baadae kupita kwenye bile duct kuelekea kwenye utumbo, na huko ndiko aina hii ya homoni ilozidi hutolewa nje ya mwili kwa kutumia nyuzinyuzi zilizoko kwenye utumbo kwahiyo unapokuwa na nyuzinyuzi  (fibers) nyingi ndivyo utaweza kukitoa kiwango kikubwa cha homoni hii iliyozidi hivyo ulaji wa vyakula vyenye nyuzinyuzi husaidia kwa kiasi kikubwa mwanamke kuepukana na tatizo hili, kwani unapokuwa na fibers chache ndivyo kiasi kikubwa cha homoni hii (oestrogen) kitakavyorudishwa mwilini.

 VYAKULA VYENYE NYUZINYUZI
vyakula vifuatavyo huwa na kiwango kikubwa cha nyuzinyuzi au fibers;
maharage
spinach
carrot
 mchicha
 kunde na jamii zakee
viazi vitamu
 matunda nk.

3. Epukana au tumia kidogo vyakula vitokanavyo na wananyama.
Vyakula hivi huwa na kiwango  kikubwa cha mafuta na hivyoo kupelekea utengenezaji wa prostaglandins
Lakini vyakula hivi havina nyuzinyuzi zozote hivyo hupelekea urudishwaji wa homoni hii ya kike kwa kiasi kikubwa kutoka kwenye utumbo.

KWA WALIO TESEKA NA TATIZO HILI KWA MDA MREFU ANZA NA NJIA HII YA NNE,  BAADA YA HAPO ENDELEA NA HIZO TATU ZA MWANZO.

4. SOY 500MG CAPSULES
Hii ni dawa asilia kabisa iliyotengenezwa kutokana na maharage ya soy na kuwekwa kitaalam katika mfumo wa vidonge dawa hii ina homoni za kike zilizotokana na mimea  (phytooetrogens).
KAZI YA DAWA HII.
1.dawa hii husaidia kubalance homoni za kike
( through NEGATIVE FEEDBACK MECHANISM) na hivyo kufanya mtu kuwa na usawa katika homoni zake na kupelekea kuepukana na tatizo hili.
2. Husaidia kupunguza matatizo yatokanayo na kikomo cha hedhi
3. Humkinga mwanamke asipate kansa zitokanazo na kuzidi kwa homoni za kike kama vile;
      Kansa ya matiti
      kansa ya shingo ya kizazi
      kansa ya utumbo nk.

NOTED :Ikumbukwe kuwa kupata maumivu wakati wa hedhi ni tatizo na sio kawaida kama inavyosemekana hivyo tumia njia hizi ambazo zinaungwa mkono na shirika la afya duniani (WHO) na shirika la kansa duniani kwani hupunguza kwa kiasi kikubwa kansa zitokanazo na KUZIDI KWA HOMONI YA KIKE

Asante Kwa kuwa pamoja nami Rafiki naomba uendelee kutembelea page hii kila siku na wape taarifa ndugu na jamaa zako waje tujifunze pamoja pia kama utahitaji Ushauri au utakuwa na la kunishauri naomba uniandikie ujumbe kupitia namba na email yangu hapo chini

KUSOMA ZAIDI MAKALA ZA AFYA TEMBELEA KATIKA BLOG HII
naythamhealthcare.blogspot.com

Imeandikwa na Dr Naytham S Masoud
Email nsalum998@gmail.com
+255623026602/+255746465095

TAFADHALI SHARE NA LIKE BLOG HII

SABABU ZA MWANAMKE KUKOSA HEDHI KWA WAKATI

FAHAMU SABABU ZA MWANAMKE KUKOSA HEDHI /KUTOPATA HEDHI KATIKA MPANGILIO MAALUMU (AMENORRHEA)

Asaalam alaykum warhmatullah wabarakatul ndugu msomaji wa page hii, napenda kukushukuru kwa kuungana Nami katika page hii kuendelea kutoa elimu kwa wanawake na wasichana kuepukana na magonjwa mbalimbali yanayosababisha kukosa hedhi iliyo salama, kutokana na maswali yenu ya kwanini mwanamke huwa anakosa hedhi ilhali Hana mimba??nimeona ni vyema kuelezea hili tatizo kwa undani ili muweze kutambua vizuri tatizo hili ambalo kitaalamu linajulikana kama AMENORRHOEA

AMENORRHEA NI NINI??
hii ni hali ya mwanamke ambaye amepevuka na kukomaa maumbile yake ya Uzaz kushindwa kupata hedhi/kupitiliza siku za hedhi
~kwa ufupi tatizo hili limekua likiwakumba na kuwaletea usumbufu wa kisaikolojia wanawake wengi wakidhani kwamba wamepata ujauzito nk, hata hivyo tatizo hili la kukosa hedhi linaweza kutokea awali au baadae kabisa maishani
~kuna aina mbili za tatizo hili (amenorrhea)

(1)PRIMARY AMENORRHEA ~hii ni hali ya kukosa hedhi inayomtokea mwanamke/msichana aliye katika umri wa kuvunja ungo ambapo Hali hii huweza kuendana na kutopata mabadiliko ya kimaumbile yanayoambatana na kuvunja ungo kama vile KUOTA NYWELE SEHEMU ZA SIRI, KUOTA MATITI, NK ila bado hapati siku zake

(2)SECONDARY AMENORRHEA ~hii ni hali ya kukosa hedhi inayomtokea mwanamke ambaye si mjamzito wala hanyonyeshi na ambaye hajakoma hedhi na wala hatumii dawa za Uzazi wa mpango ambapo awali alikua akipata hedhi kama kawaida Lakini akasimama kwa muda huenda ni miezi au mwaka mzima hapati hedhi mpaka sasa

~NAMNA AMBAVYO MWANAMKE HUPATA HEDHI
Kwa Kawaida ili mwanamke apate hedhi katika mzunguko ulio Sawa ni lazima tezi ya hypothalamus na pituitar pamoja na kiwanda cha mayai(ovaries) viwe vinafanya kazi kwa ushirkiano yani sawasawa

~VYANZO VYA TATIZO HILI
Vyanzo vya tatizo hili vyaweza kuwekwa katika Makundi makuu matatu ambayo ni vile vinavyohusisha matatizo katika mfumo wa homoni, vile vinavyohusisha matatizo katika tezi ya pituitar, mfumo wa Uzazi na vile vinavyohusisha mabadiliko katika mwili wa mwanamke visababishi hivyo ni ÷
👉matatizo katika hypothalamus ambapo matatizo haya husababisha ÷uvimbe katika ubongo karibu na tezi ya pituitar, ukosefu au upungufu wa homoni zinazochochea kukua na kufanya kazi kwa via vya Uzazi,

👉uzito mdogo kuliko Kawaida

👉pituitar kushindwa kufanya Kaz vzur baada ya seli zake kufa hii ni iwapo mama alipoteza damu nyingi wakati wa kujifungua

👉kuwepo kwa kiwango kikubwa cha homoni ya prolactin katika damu (PROLACTINEMIA)
(proclatin ni homoni inayochochea uzalishaji wa maziwa wakati wa kunyonyesha hivyo Hali ya kuwa proclatin nyingi katika damu husababisha kukosa hedhi

👉kuwa na msongo wa mawazo ni hatari

👉kuziba kwa utando unaozunguka uke (HYMEN) hivyo kukosekana tundu la kupitishia damu (IMPERFORATE HYMEN)

👉 Mazoezi makali ya mwili na ulaji mdogo wa Chakula, tabia hii hushusha homoni ambayo inahusika na kuweka siku zako katika Hali nzuri yani hufanya leptin kuwa katika kiwango cha chini sana hivyo ni hatari

👉ugonjwa wa kurithi wa GALACTOSEMIA unaoambatana na kuwa na kiwango kidogo cha sukari aina ya GALACTOSE katika damu

👉baadhi ya magonjwa ya viungo vya Uzazi yamekua yakiambatana na kusimama kwa hedhi mfano wa magonjwa hayo ni POLYCYSTIC OVARIAN SYNDROME

👉MENO PAUSE ~hii ni hali ambayo hutokea kipindi cha miaka 42_55 homoni zinazohusika na kupata hedhi huwa Kwenye kiwango cha chini sana kiasi hufanya haziwezi kufanya Kazi sawasawa

DALILI ZA TATIZO HILI
👉Mwanamke kuwa na vinyweleo vingi na kuota ndevu hii inamaanisha na kuashiria kuwepo kwa kiwango kikubwa cha homoni za kiume za ANDROGEN

👉kuongezeka uzito kupita kiasi

👉matiti kutoa maziwa wakati mwanamke si mjamzito wala hanyonyeshi

👉mwanamke kuwa na mhemko kuliko Kawaida

👉 uke kuwa mkavu

👉kutokwa jasho sana wakati  wa usiku

👉mabadiliko katika kupata usingizi vinaweza kuashiria kuwepo kwa tatizo katika ovaries

👉kutokupata hedhi katika mpangilio

MATIBABU
NA JINSI YA KUJIKINGA NA TATIZO HILI
matibabu ya kukosa hedhi yanaweza kutibiwa hospital kutokana na chanzo cha tatizo ambapo huwa ni kupewa dawa au kufanyiwa upasuaji pale patapobidi

NOTE :Ni vizuri kuongea na daktari ili ajue ni kwa namna gan atakusaidia pia waweza kufanya mambo yafuatayo ili kujiepusha na tatizo hili

👉ZINGATIA ULAJI ULIOSAHIHI AMBAO UNAHUSISHA ULAJI WA MATUNDA KWA WINGI NA MBOGA ZA MAJANI

👉TUMIA MAZIWA YA SOY /JUICE YA WATERMELON/MAJI YA MSHUBIRI

👉FANYA MASAJI KWENYE TUMBO LA CHINI KWA KUTUMIA MAJI YA UVUGUVUGU (UKIWA KTK BREED) HII ITASAIDIA KUONGEZA DAMU NYINGI KUTOKA

👉KULA CHAKULA  KISICHOTOKANA NA DAMU (VEGETARIAN DIET) CHENYE PROTIN NYINGI MFANO, NAZI, MAHARAGE, KOROSHO NA KARANGA
Hakikisha unazingatia haya ili kuepukana na madhara ya huu ugonjwa ambayo ni makubwa sana

MADHARA YANAYOWEZA KUTOKEA IWAPO TATIZO HILI HALITAPATIWA MATIBABU
👉Mwanamke kuchelewa kuingia menopause hali huu ni mbaya kwani husababisha SARATAN YA MATITI kwa kias kikubwa
👉mwanamke kupata maumivu wakati wa tendo la ndoa kwasababu ya kupungua kwa hamu ya kufanya mapenzi na uke kuwa mkavu
👉husababisha matatzo ya kutopata usingizi
👉matiti husinyaa na kupata hedhi Bila mpangilio,

ndugu Rafiki msomaji Asante kwa kuwa Nami muda wote kutoa elimu hii kwa jamii kama una MAONI/ USHAUR NIANDIKIE UJUMBE KUPITIA NAMBA NA EMAIL YANGU HAPO CHINI

KUSOMA ZAIDI MAKALA ZA AFYA TEMBELEA BLOG HII
naythamhealthcare.blogspot.com

Makala hii imeandaliwa na Dr Naytham S Masoud
email-nsalum998@gmail.com
+255623026602/+255746465095

PLEASE USISAHAU KUSHARE, KUKOMENT, KULIKE NA KUWAALIKA WENZAKO KATIKA PAGE HII NI VIZURI ZAIDI UKISHARE NA WENZAKO WAPATE ELIMU HII

TATIZO LA UVIMBE KATIKA KIZAZI CHA MWANAMKE (UTERINE FIBROID/LEIO MYOMAS)

FAHAMU UVIMBE KATIKA KIZAZI CHA MWANAMKE (UTERINE FIBROIDS/LEIO MYOMAS)

Asalaam alaykum warhmatullah wabarakatull
Natumaini mnaendelea vizuri, leo tena napenda kuzungumzia tatizo la uvimbe katika kizazi tatizo(UTERINE FIBROIDS/LEIO MYOMAS) ambalo ni common  kwa wanawake wengi

FIBROIDS NI NINI??
~Ni Aina ya vivimbe vinavyoota kwenye misuli Laini ya mfuko wa uzazi
~tatizo hili huwakumba wanawake wengi ambapo huwapata kwa 5% wanawake wenye umri wa miaka 20_30 na 20% kwa wanawake wenye umri wa miaka 30_40 na zaidi ya 40% ni kwa wale wenye umri zaidi ya 40 hivyo kwa ujumla tatizo la fibroids huwapata wanawake wengi hasa katika umri wa kuzaa (reproductive age) hii inamaana kuwa kadri umri unavyokuwa mkubwa mwanamke ana nafasi kubwa ya kupata uvimbe.
~tafiti zinaonyesha kuwa tatizo hili huwapata zaidi wanawake wa kiafrika kuliko wazungu pia huwapata zaidi wanawake ambao hawajazaa kabisa au wale ambao wamekaa Muda mrefu Bila kuzaa, pia wanawake wanene, na wale waliopata hedhi mapema wapo katika hatari ya kupata ugonjwa huu

AINA KUU ZA FIBROIDS
~(1)SUBMUSOCAL FIBROIDS ~hii hutokea ndani ya kizazi
~(2)INTRAMURAL FIBROIDS ~hii hutokea ndani ya nyama ya kizazi
~(3)SUBSEROL FIBROIDS ~hii hutokea nnje kwenye ukuta wa kizazi
~uvimbe huwa na ukubwa tofauti kwani huanza mdogo na baadae kuwa mkubwa sana na hata wakati mwingine mwanamke huweza kuonekana mjamzito, kwani uvimbe huu huweza kuwa mmoja mkubwa na wakati mwingine huwa zaidi ya mmoja na kutanda katika mfuko wa kizazi
~watu wengi wamekuwa wakihisi fibroids kitu ambacho sio kweli kwasababu fibroids sio kansa Bali ni uvimbe wa kawaida ambao hukua kwa kutegemea kichocheo au hormone ya OESTROGEN na ndio maana wakati wa kupata tatizo hili huwa ni kipindi cha kubalehe mpaka kukoma kwa hedhi

CHANZO CHA TATIZO
~Chanzo halisi cha ugonjwa huu hakijafanikiwa kuwa wazi ila Kuna sababu ambazo huweza kusababisha mwanamke kupata fibroids, sababu ambayo ni common kusababisha tatizo hili ni WINGI WA HOMONI YA OESTROGEN ambayo ipo katika mwili wa mwanamke na ndiyo hufanya Kazi  ya kusababisha mwanamke kupata hedhi pia mara nyingi uvimbe huu hukua mkubwa sana kipindi cha UJAUZITO kwasababu vichocheo vya OESTROGEN huongezeka na kuwa vingi ili kulinda makuzi ya mtoto pia ni mara chache watu walio kikomo cha hedhi kupata fibroids na wakipata Kuna hatari ya kuwa kansa
DALILI ZA FIBROIDS
~dalili za uvimbe katika kizazi cha mwanamke hushindwa kuonekana iwapo uvimbe ni mdogo na pia dalili hutegemea sehemu ilipo kwenye mfuko wa kizazi pia na ukubwa wake, pamoja na hayo dalili zake mara nyingi ni zifuatazo ÷
👉KUTOKWA NA DAMU YENYE MABONGE MABONGE KWA MUDA MREFU
👉KUTOKWA DAMU KATIKATI YA MWEZI NA HEDHI KUTOKUWA NA MPANGILIO
👉KUPATA MAUMIVU YA KIUNO HASA WAKATI WA HEDHI
👉KUPATA MAUMIVU MAKALI WAKATI WA TENDO LA NDOA
👉KUPATA MAUMIVU MAKALI YA MGONGO
👉KUKOJOA MARA KWA MARA
👉MIMBA KUHARIBIKA MARA KWA MARA
👉KUPUNGUKIWA NA DAMU MARA NYINGI
👉MIGUU KUVIMBA
👉MKOJO KUBAKI KWENYE KIBOFU
👉HAJA KUBWA KUWA NGUMU
👉UGUMBA

MATIBABU &  VIPIMO
~matibabu ya fibroids hufanyika kwa daktari kumkagua mgonjwa kwa kutumia mikono miwili au kupima (Bimanual examination) pia anaweza kutumia kipimo cha ULTRA SOUND ya nyonga kwani ni rahis kugundua uvimbe au kipimo cha MRI,
~matibabu huweza kulenga ya kutibu dalili au kupunguza uvimbe na pia iwapo mwanamke ana tatizo hili na hamna dalili zozote basi anaweza kufuatilia tu uvimbe Bila kutumia dawa kwasababu mwanamke anapofikia menopause (kukoma hedhi)  tatizo hili hutokewa
~wanawake wengi wana fibroids ndogo ndogo ambazo hazina dalili hivyo hushindwa kutambua mpaka pale wanapobeba ujauzito au kupima ndio hugundulika
~NJIA ZA KUTIBU UVIMBE MKUBWA
~(1)DAWA
~hapa mgonjwa hupewa matibabu ya dawa ambazo hurekebisha kiwango cha homoni ya OESTROGEN mfano wa dawa hizo ni DANAZOL,na Aina ya pili ni vidonge vya kutuliza maumivu ya fibroids
~(2)UPASUAJI
Upasuaji hufanyika kwa kutegemea na ukubwa wa uvimbe na wingi wa fibroids ambapo upasuaj huo ni wa Aina mbili
(A) MYCOMECTOMY ~hii ni njia ya Upasuaji hutumika kwa mgonjwa mwenye uvimbe mmoja mkubwa ulio katika sehem nzuri na Upasuaji huu ni kutoa uvimbe tu na kuacha kizazi hata hvyo Upasuaji wa njia hii uvimbe una nafasi kubwa ya kurudi
(B) TOTAL ABDOMINAL HYSTERECTOMY ~hii ni njia ya Upasuaji ambapo kizazi hutolewa na hufanyika ikiwa kizazi kina uvimbe mmoja mkubwa sana au vivimbe vikiwa vingi vingi

MADHARA MAKUBWA YA FIBROIDS
~Husababisha mimba kutoka mara kwa mara na hatimaye mtu kuwa mgumba, pia huweza kusababisha saratani ya shingo ya kizazi
NOTED :ndugu rafiki hakikisha unaenda kupima Afya yako kila mwezi ili kujua maendeleo ya Afya yako kwani wengi huwa hawajitambui kuwa Wana tatizo hili la fibroids
IKIWA UNA MAONI/MASWALI/MAPENDEKEZO YOYOTE NIANDIKIE KUPITIA E-MAIL NA NAMBA YANGU HAPO CHINI

PIA KUSOMA ZAIDI MAKALA MBALIMBALI ZA AFYA TEMBELEA NAYTHAMHEALTHCARE.BLOGSPOT.COM

Makala hii imeandaliwa na Dr Naytham email:nsalum998@gmail.com
+255623026602/+255746465095
PLZ USISAHAU KUSHARE, KUKOMENTI, KULIKE NA WATAG RAFIKI ZAKO