BREAKING
  • FANGASI UKENI

    Pata suluhisho la tatizo la fangasi ukeni pamoja na ushauri utakaokufanya uwe salama daima

  • TIBA YA NGUVU ZA KIUME

    Okoa nyumba yako kwa kupata dawa itakayo ongeza nguvu zako za kiume na kudumisha unyumba daima

  • SULUHISHO LA U.T.I

    Je hauna ufahamu wowote kuhusu U.T.I ?Je Unakabiliwa na tatizo la U.T.I?Wasiliana nami nikujuze zaidi huenda una tatizo la U.T.I lakini haujijui,na kama unalo basi tiba yake ipo

  • TIBA YA VIDONDA VYA TUMBO

    Je Umesumbuliwa na vidonda vya tumbo kwa muda mrefu pasina kupata suluhisho,wasiliana nami nikupatie dawa itakayoondoa tatizo lako kabisa

BannerFans.com

Jumatatu, 17 Agosti 2015

TIBA YA UGONJWA WA KUOTA KINYAMA SEHEMU ZA SIRI NA SEHEMU MBALIMBALI ZA MWILI (GENITAL WARTS & SKIN) IMEPATIKANA WAHI MATIBABU SASA!!!

FAHAMU UGONJWA WA MASUNDOSUNDO AU KUOTA VINYAMA SEHEMU ZA SIRI (GENITAL WARTS & SKIN)
Asalaam alaykum warhmatullah wabarakatul natumaini mnaendelea vizuri leo napenda kuzungumzia tatizo la kutokewa vinyama katika sehemu za siri na mwili au Masundosundo au vigwaru kwa kitaalamu tunauita GENITAL WARTS
~GENITAL WARTS ni nini?!!
~ni ugonjwa wa kuota vinyama Laini vidogovidogo vinavyoota kwenye ngozi au utando Laini unaozunguka maeneo ya sehemu za siri.
~vinyama hivyo vinaweza kutokea kwenye uume, uke, mrija wa mkojo (urethra), vulva, na shingo ya kizazi au maeneo yanayozunguka haja kubwa, ugonjwa huu huenezwa kwa njia ya kujamiiana (SEXUAL TRANSMITTED INFECTION (STI)
CHANZO CHA TATIZO HILI
Ugonjwa wa Masundosundo husababishwa na virus waitwao HUMAN PAPILLOMA VIRUS (HPV) hata hivyo Kuna Aina 70 tofauti za virus wa HPV hivyo sio wote wanaosababisha tatizo hili kwani Kuna ambao wanasababisha Masundosundo katika mwili sehemu tofauti kama vile mikono, miguu, mgongoni, NK pia wapo wanaosababisha saratani ya shingo ya kizazi (CARCINOMA OF THE CERVIX),saratani ya uume na saratani ya njia ya haja kubwa (ANAL CANCER) kwa jinsia zote mbili
°ugonjwa huu wa Masundosundo umejitokeza kwa kiasi kikubwa baada ya kuwepo kwa janga la UKIMWI hivyo watu wenye wapenzi wengi, wanaofanya mapenzi kwa njia ya haja kubwa, wajawazito, watumiaji wakubwa wa sigara na pombe, watu wanaofanya mapenzi kwa njia ya mdomo Wana hatari ya kupata tatizo hili.
DALILI ZA MASUNDOSUNDO
👉mgonjwa wa tatizo hili hutokewa na vinyama Laini vidogovidogo vinavyojitokeza juu ya ngozi katika maeneo tofauti (MFANO HALISI TIZAMA KATIKA PICHA HIZO) ingawa wakati mwingine huwa ni vidogo kiasi cha kutoweza kuonekana kwa njia ya kawaida
👉mgonjwa kupata ganzi maeneo yaliyozungukwa na Masundosundo
👉kutokwa na uchafu sehem za siri na kuwashwa kupita maelezo
👉kutokwa damu ukeni mara baada ya kufanya tendo la ndoa MATIBABU NA JINSI YA KUEPUKA UGONJWA HUU
°matibabu ya tatizo hili hupatikana kirahisi nchini Tanzania na tiba hutolewa kwa kufuata utaratibu wa Majibu yaliyopatikana katika vipimo mbalimbali ambapo matibabu huwenda kuwa kufanyiwa operation kuondoa vinyama ingawaje tiba hii haina ufanisi mzuri kwasababu huweza kutengeneza madhara zaidi na uwezekano mkubwa wa kupata kansa hivyo tiba nzuri ni kutumia dawa ambazo zitatibu na kuondoa tatizo hilo na mgonjwa kupona kabisa ila cha kuzingatia ni kwamba ugonjwa huu ni wa kuambikiza hivyo inashauriwa wenza wote kupata matibabu hata kama atajihisi hana dalili yoyote ni vyema akafanya vipimo ili kujihadhari kabla ugonjwa haujaleta madhara zaidi na uwezekano mkubwa ~Waswahili wanasema bora kinga kuliko matibabu hivyo ni bora ukaepuka ugonjwa huu kwa kuepuka yafuatayo
👉EPUKA KUWA NA WAPENZI WENGI
👉EPUKA KUFANYA MAPENZI KINYUME NA MAUMBILE
👉EPUKA KUTUMIA DAWA ZA KULEVYA, SIGARA NA POMBE
👉ACHA ORAL SEX KAMA UTASHINDWA BASI KUA NA MPENZI MMOJA TU UTAKAYEKUA UNAMNYONYA SEHEMU ZA SIRI ZINGATIA MAPENZI NI UJUZI LAKINI AFYA YAKO NI MALI ZAIDI WADADA /WAKAKA WENGI MMEKUA MKIFANYA HIVI KWA LENGO LA KUWARIDHISHA KILA MNAOKUTANA NAO KIMWILI KITU KINACHOKUWEKA KATIKA HATARI YA KUPATA TATIZO HILI AU KANSA YA KOO
NOTED :NDUGU RAFIKI Ugonjwa huu una madhara makubwa unaweza kusababisha kansa ya kizazi, kansa ya uume, kansa ya njia ya haja kubwa NK hivyo ni vyema ukapata matibabu ya uhakika iwapo una tatizo hili na kama hauna tatizo hili ni vyema ukajiepusha na ugonjwa huu
NDUGU RAFIKI KAMA UNA TATIZO/MASWALI /MAONI NIANDIKIE KUPITIA email nsalum998 @gmail.com au text me kwa namba 0689538628
PLZ USISAHAU KUSHARE, KUKOMENT NA WATAG RAFIKI ZAKO WAJIFUNZE 

Jumatano, 12 Agosti 2015

JE, UNAYAJUA MADHARA YA KUKOSA CHOO KWA MUDA MREFU? ??

FAHAMU ATHARI YA TATIZO LA KUTOPATA CHOO NA NAMNA YA KUEPUKA TATIZO HILI 
Habari za leo rafiki ni matumaini yangu unaendelea vyema na kufurahia uwepo wa blog hii, Nimepokea email nyingi kuhusu tatizo la kutopata choo hvyo nimeona ni heri kuzungumzia hapa ili wote mfahamu tatizo hili 
~tatizo Hili ni sugu sana miongoni mwa watu wengi na kwa watoto wadogo pia  Bila kujua ni tatizo ambalo linahitaji tiba ya haraka hata hivyo wengi huwa wanapuuzia na kuona ni tatizo la kawaida, LAHASHA!!! Napenda kukuambia rafiki tatizo la kutopata choo kwa Muda mrefu ndio chanzo cha magonjwa mengine tena ya hatari zaidi kwasababu mtu unapokosa choo kikubwa kwa siku kadhaa uchafu unaotakiwa kutoka hujikusanya tumboni na unapokosa sehemu ya kutokea unahamia kwenye damu na kuwa sumu na chanzo cha maradhi mengine ambayo hujitokeza baadae na kukuathiri zaidi 
~kwa kawaida mtu anapaswa kupata choo cha uhakika japo mara moja kwa siku na mara Tatu kwa wiki hivyo iwapo unakosa choo kwa siku Tatu ilhali unakula elewa moja kwa moja una tatizo katika mfumo wa mmeng'enyo 
CHANZO CHA TATIZO HILI LA KUTOPATA CHOO 
~tatizo hili husababishwa zaidi na ulaji mbovu wa vyakula na kutokujizoesha kwenda haja mara kwa mara pia kula vyakula vilivyokobolewa na matumizi mabaya ya dawa na magonjwa mengine pia mabadiliko ya hormone 
DALILI ZA KUTOPATA CHOO 
~dalili za tatizo hili ni ÷
👉KUPATA HOMA KALI 
👉KUTETEMEKA KWA BARIDI 
👉KUTUMIA NGUVU NYINGI NA MUDA MWINGI KUJISAIDIA 
👉ULIMI KUWA NA UTANDU MWEUPE NA KUTOA HARUFU MBAYA 
👉KUKOSA HAMU YA KULA 
👉TUMBO KUJAA GESI 
👉KUPATA VIDONDA SEHEMU YA NNJE YA HAJA KUBWA 
NAMNA YA KUTIBU NA KUEPUKA TATIZO LA KUTOPATA CHOO 
~matibabu ya tatizo la kutopata choo kwa ufup ni magumu na marahisi pia kutokana na ukubwa wa tatizo pia hata hivyo kila mtu anaweza kujikinga na tatizo hili kwa kufuata kanuni za ulaji wa lishe bora kwasababu tatizo la kutopata choo husababishwa na namna unavyokula au kuishi hivyo ukifuata kanuni za lishe bora tatizo hili halitakupata hivyo njia sahihi ya kujikinga na tatizo la kutopata choo ni kula nafaka zsizokobolewa, matunda, mbogamboga na maji kwa wingi 
~matibabu hufanyika kwa kuangalia ukubwa wa tatizo na Hali ya mhusika kwan matibabu ya mtoto sio sawa na ya mtu mzima mwenye miaka 70 Hali kadhalika tatizo hili likijulikana mapema huwa rahisi kulikabili tofauti na tatizo la mda mrefu ambapo tiba Yake huweza kuwa kubwa haswa ambapo tiba Yake huhusisha vidonge na chakula na hata kufanyiwa upasuaji kuondoa kinyesi kilichoganda katika damu na kuendelea na matibabu ya chakula 
MADHARA YA KUKOSA CHOO KWA MUDA MREFU 
~madhara ya kukosa choo kwa Muda mrefu ni÷
👉KUPATA SARATANI YA UTUMBO 
👉FIGO KUSHINDWA KUFANYA KAZI VIZURI 
👉KUPATA PRESHA NA KUPATA UGONJWA WA INI 
👉KUPATA MAGONJWA YA MOYO NK 
KUMBUKA :zingatia kula milo mitatu kila siku, kula vyakula vyenye nyuzinyuzi nyingi (high fibre diet), kunywa maji mengi na fanya mazoezi mara kwa mara pia usizoee kutumia dawa za kemikali ovyo ovyo ovyo 
NDUGU RAFIKI KAMA UNA TATIZO LA KUTOPATA AU NDUGU YAKO ANA TATIZO HILI KWA MUDA MREFU WASILIANA NAMI 0689538628 KWA USHAURI WA MATIBABU ZAIDI 
JE, UMEJIFUNZA???!! ! BASI SHARE NA WENZAKO WAJIFUNZE  

Jumatatu, 29 Juni 2015

HIZI NDIO FAIDA ZA KUNYWA MAJI GLASS SABA MWILINI



Suala la kunywa maji tumekuwa tukihimizwa kila mara na wataalamu wa Afya. Lakini zoezi hili limekuwa gumu kwa kuwa watu wengi huona kama adhabu. Imekuwa ikihimizwa angalau kunywa Lita mbili(2) za maji kila siku kwa kila mtu.
Nimekuwa nikiwasikia watu wengi wakidai wameenda Hospitali kutibiwa wameambiwa wanywe maji ya kutosha ili yawasaidie. Pia wengine wakithubutu kusema kuwa ukinywa maji mengi basi waweza tibu ugonjwa wa UTI kirahisi kabisa. Hili ni kweli lakini tatizo watu wengi hatuwezi kunywa hayo maji mengi.
Leo nitakupa mpangilio rahisi kabisa wa kunywa maji glass 7 kwa siku na faida zake mwilini. Hii itakusaidia zaidi maana glass 7 ni sawa na Lita 2 karibu na nusu.
GLASS 1. kunywa maji glass moja mara baada ya kuamka. Hii husaidia viungo vya ndani vya mwili kama figo, moyo, n.k
GLASS 1. Nusu saa kabla ya kunywa chai. Husaidia katika mmeng'enyo wa chakula
GLASS 1. Kabla ya kuoga asubuhi. Husaidia kushusha shinikizo la moyo
GLASS 1. Nusu saa kabla ya chakula cha mchana. Pia husaidia katika mmeng'enyo wa chakula
GLASS 1. Kabla ya kuoga jioni. Pia husaidia kushusha shinikizo la moyo
GLASS 1. Nusu saa kabla ya chakula cha usiku. Vilevile husaidia katika suala la mmeng'enyo wa chakula
GLASS 1. Kabla ya kulala. Husaidia kuepuka kupata shambulio la moyo
Hiyo ndiyo ratiba nzuri ya kunywa maji glass 7 bila kuhangaika.

VIJUE VYAKULA VINAVYOPELEKEA KISUKARI MWILINI

Ndugu karibu sana katika makala zangu ambazo huzungumzia chanzo cha tatizo, namna ya kuepuka na kutibu kabisa hilo tatizo bila kukaa kuhangaikia kutibu dalili ya ugonjwa. Ni dhahili kuwa maisha yetu ya kifahari tumekuwa tunakula vyakula vyakutosha lakini vyakula hivi si vyakujenga mwili bali vinakuja na magonjwa mengi ndani yake. Siwezi kuilaumu jamii kwa kuendelea kula vyakula hivi bila kuwa na kiasi bali ni mfumo wa afya kwa ujumla ambayo inaweka juhudi kubwa kubaini magonjwa na kutibu dalili na siyo kuweka jitihada kubwa katika kutoa elimu ya namna ya kujikinga na magonjwa na kushughurika na chanzo au mzizi wa ugonjwa. Hivyo ni jukumu letu kuhakikisha jamii inaepukana na magonjwa haya kwani tukifanya hivyo utamaduni huu wa kutuletea vyakula vinavyo dhoofisha miili yetu na hatimaye wanaleta misaada ya matibabu inayo lenga kubaini magonjwa na sio kutoa elimu ya kuzia na kupambana na vyanzo hasa vya tatizo.
Baada ya kusema hivyo basi ningependa kwa siku ya leo nizungumzie kidogo madhara ya vyakula vyenye sukari nyingi na nguvu za kiume ambazo hadi sasa wanaume ambao hawawezi kutungisha mimba idadi inaongezeka. Kumekuwa na usemi kuwa upungufu wa nguvu za kiume unahusishwa sana na kuzeeka kwa mtu. Ni dhahiri kuwa kuzeeka kwako sio chanzo cha wewe kupata upungufu wa nguvu za kiume na hutakiwi kuhusisha bali ni tabia yako inayo ambatana na ulaji wa vyakula na unywaji wa vinywaji vyenye sukari nyingi,unywaji pombe,uvutaji sigara, utumiaji wa madawa ya hospitali bila ushauri maalumu na pia utumiaji madawa ya hospitali pale unapotibu ugonjwa flani kwa mfano dawa za kifafa, dawa za usingizi na dawa za dege dege,utumiaji wa madawa ya kulevya na kujichua kila siku. Hivyo maisha yetu ya kila siku ndio chanzo cha ukosefu wa nguvu za kiume
NINI MCHANGO WA VINYWAJI VYENYE SUKARI NYINGI NA VYAKULA VYA VIWANDANI KATIKA UPUNGUFU WA NGUVU ZAKIUME
Tumekuwa tukiishi mazingira ya kula vyakula vya sukari kila siku kwa mfano, ukiamka asubuhi unakula mikate, tafiti zinasema kuwa mkate una aina ya wanga iitwayo amylopectin A ambayo endapo ikimeng”enywa ni chanzo cha sukari nyingi sana kwenye damu. Pia unatakiwa kufahamu kuwa slice mbili za mikate ni sawa kama umeramba vijiko viwili vya sukari ya mezani yani sukari nyeupe. Hivyo mikate ni moja ya vyakula vyakuepuka sana kama unahitaji kuwa na afya njema na mwenye nguvu za kiume tele. Pia imekuwa ni kawaida unaamka asubuhi na soda kwani hii ni ishara kuwa tayari kiini mahususi kwenye soda ambacho huitwa ASPARTAME kimesha kuaathiri na umekuwa addicted na vyakula vya sukari. Aspartame ni kiambata mahususi kwenye vinywaji vya coka na hivyo kimewekwa humo ili kukufanya uwe na hamu ya kunywa soda mara kwa mara au kula vyakula vitamu vitamu. Kiini hiki huenda kwenye ubongo na kujishika kwenye vipokea taarifa yani receptors na kutoa taarifa ambazo zina angamiza mwili wako.
Sukari inapozidi mwilini inasababisha uchovyaji wa insulin kwa wingi ambayo hupunguza kiasi cha testosterone ndani ya ndamu na hatimaye kupunguza nguvu na shauku ya tendo la ndoa. Kulingana na utafiti uliofanywa kwa kutumia kipimo cha sukari kiitwacho ORAL GLUCOSE TORELANCE TEST AU OGT kilionesha kuwa wanaume wenye sukari nyingi kwenye mzunguko wa damu walionesha kiwango kidogo cha kichocheo cha nguvu za kiume kiitwacho testosterone ambacho hushughurika na sifa za kiume,kutengeneza mbegu za kiume na kuimarisha misuli bila kusahau nguvu za kiume. Ni dhahili kuwa ongezeko kubwa la wanaume ambao wana matatizo ya nguvu za kiume inasababishwa na ulaji na unywaji wa vyakula vyenye sukari nyingi. Hivyo basi ni dhahiri kuwa kama una tatizo hilo linaweza kukupelekea kukosa mototo kwani hata manii ya kiume kutengenezwa kwake itakuwa ni kwa shida sana. Epuka hivi vyakula na jua namna gani unaweza rudisha afya yako mwanzo kwa kutumia vyakula na virutubisho mahususi vinavyo ondoa tatizo la nguvu za kiume.
Pia vyakula vya sukari nyingi hupunguza kwa hali ya juu vichocheo vya kujenga mwili yani GROWTH HORMONE ambayo hutolewa na tezi ya pituitary wakati wa usingizi mzito. Kichocheo hiki cha kujenga mwili yani GROWTH HORMONE kinafanya kazi kubwa ya kutumia mafuta yaliyohifadhiwa kwa matumizi ya ziada, pia growth hormone huimarisha misuli ya mwili na kuimarisha nguvu za kiume. Hivyo kupungua kwa kichocheo hiki husababisha mrundikano wa mafuta mabaya na kutengeneza nyama zembe yani BELLY FAT, kuongezeka uzito,kupata kizuizi cha insulin na hatimaye kisukari aina ya pili.
Vyakula vya sukari nyingi hukufanya muda wote ujihisi umechoka na huna nguvu ya kufanya kazi yoyote na wengine hufikiria kuwa wanasumbuliwa na ugonjwa wa malaria. Hii ni kwa sababu sukari nyingi kupita kiasi inasababisha utoaji wa insulin kuongezek a ili kupunguza sukari hiyo na matokeo yake kusababisha njaa na shauku ya kula mara kwa mara kwa sababu ya kupungua kwa reptin hormone inayotolewa na seli za kuhifadhi mafuta. Pia sukari nyingi huzuia utengenezwaji wa kichocheo kiitwacho OREXIN ambacho husafirisha taarifa na kuongoza kitendo cha ulaji na kukufanya uwe na nguvu ya kuwa macho na kufanya kazi zako. Sasa orexin inapopungua inasababisha muda wote kukaa umechoka na unasinzia ovyo ovyo. Ni dhahiri kuwa inaweza kuwa unasema hii makala ni miongoni mwa waathiriwa wa sukari nyingi kwani uzito umekuzidi,kitambi,unasinzia ovyo ovyo na muda wote umechoka. Usihofu na usikate tama chakula cha matunda na mboga mboga ndio suluhisho lako kama wewe huwezi kutumia hivi basi jitahidi kutafuta virutubisho vyenye kurudisha afya yako upya bila usumbufu kabisa.
Pia sukari nyingi kwenye damu husababisha msongo wa mawazo sana na hatimaye kusababisha utolewaji wa vichocheo vya CORTISOL ambayo husababisha ulaji ovyo wa vyakula wa bila mpangilio. Mtu kama huyu utakuta unakula pale pale baada ya muda mfupi tena njaa. Hivyo tujifunze namna gani sasa unaweza kuirudisha afya yako bila tena kuendelea kuongeza sumu mbali mbali mwilini. 
Napenda nikupongeze msomaji wangu ni jukumu lako kujua nini cha kufanya kama wewe bado ujafikia ku athiriwa na tatizo hili. Hivyo basi nina imani utailinda afya yako na kuipenda. Chakula cha mimea na matunda kinakuweka mbali na dawa hizi wapenda kwani tusipende kula vyakula vyenye nembo ya kuisha muda wake. Kwa Yule tayari ameshakubwa na tatizo hili kwa sababu ya matumizi ya sukari nyingi napenda kukuambia kuwa CHAKULA PEKEE NI TIBA KABISA NA KUJIEPUSHA NA DAWA ZA KILA SIKU UNAZO NUNUA AMBAZO HAZITIBU TATIZO. Kama huwezi kupangilia chakula chako vizuri na namna ya kurudisha tatizo lako unaweza tumia viutubisho vinavyo ondoa tatizo na kurudi kuwa kijana. Kama ukihitaji tunaweza kukuelekeza namna ya kukipata au tupigie

JE UNASUMBULIWA NA MATATIZO YA MAUMIVU YA MGONGO????SOMA MAKALA HII




Maumivu chini ya mgongo hutokea sana kwa kila mtu na mara nyingi huwa ni chini ya mbavu za nyuma na juu ya miguu na huweza kusambaa mpaka kwenye kiuno na hips. Maumivu haya usikika na kuumiza pale unapoinua kitu, kusimama, kukaa kwenye kiti au kutembea na usababishwa na matumizi kupita kiasi ya misuli, kano, mishipa na neva za mgongoni au kwenye pingili za uti wa mgongo kutokana na kugandamizwa sana. Pia huweza kusababishwa na kuvunjika au maambukizi katika pingili za uti wa mgongo, umri mkubwa, saratani ya mifupa,uzito kupita kiasi mawe katika figo, uvimbe na saratani ya kizazi .

TIBA YAKE
Unaweza kujifanyia huduma ya kwanza mwenye kwa kutumia dawa za kupunguza maumivu, kuchua, kuweka barafu au joto kiasi, kufanya mazoezi mapesi na kukaa au kulala mtindo unaopunguza maumivu.
Punguza uzito, epuka kuanguka mara kwa mara na usibebe mizigo mizito kupita kiasi au kaza sana tumbo unaponyanyua mizigo mizito
Usizunguke wakati au kuinamia mbele wakati umebeba vitu vizito
Usisimame kwa kubana miguu muda mrefu
Maumivu yakizidi fika hospitali ili kufanyiwa uchunguzi na vipimo vya X rays, CT scan na MRIs kwa ajili ya kugundua tatizo na kupata tiba zaidi.
0689538628 KWA MAELEZO ZAIDI NA TIBA WASILIANA NAMI 

Alhamisi, 18 Juni 2015

TATIZO LA KUTOPATA USINGIZI MZURI (ISOMNIA)

TATIZO LA KUTOPATA USINGIZI MZURI (ISOMNIA)
Habari za leo ndugu msomaji wa blog hii ni matumaini yangu unaendelea vizuri na kufurahia blog yangu,nimekua nikiona watu wengi wakisumbuliwa na (insomnia) tatizo la kutokupata usingizi vizuri wakati wa usiku na wao kuona Hali hii ni ya kawaida wakati Hili ni tatizo na Lina madhara makubwa sana kwa mhusika,
 ~ISOMNIA (KUKOSA USINGIZI)_huu ni ugonjwa ambao unaambatana na tabia tofauti ambazo ni KUSHINDWA KUPATA USINGIZI KABISA, KUBADILIKA KWA MFUMO WA KULALA, KUSINZIA HARAKA BAADA YA KUPANDA KITANDANI,  NA USINGIZI KUISHA NA KUSHINDWA KULALA TENA BAADA YA KUSHTUKA,
 _Ugonjwa huu ni hatari sana kwa afya yetu kwasababu huathiri mfumo mzima wa mwili, mathalani Mbali ya kuathiri Kinga ya mwili pia huongeza hatari ya kupata magonjwa hatarishi
 VIHATARISHI /VISABABISHI VYA UGONJWA WA ISOMNIA
 visababishi vya ugonjwa huu vipo vingi sana hivyo yatupasa kuviepuka ili kujiepusha na huu ugonjwa.zifuatazo ni visababishi vya ugonjwa huu
 đź‘‰Utumiaji wa madawa kama cocain, nicotine, cafein, na unywaji wa pombe uliopitiliza
 đź‘‰upungufu au ongezeko la homoni za Uzazi hasa katika kipindi cha uzee kwa wanawake (menopause)
 đź‘‰magonjwa ya moyo ambayo humfanya mtu ashindwe kupumua vizuri wakati wa kulala
 đź‘‰Utumiaji wa madawa za kuleta usingizi kama vile DIAZEPAM/VALIAM
 đź‘‰matatizo ya mfumo wa Chakula kama vile kiungulia na kupata choo kigumu
 đź‘‰kuwa na MSONGO wa mawazo
 đź‘‰mazingira mabaya ya kulala mfano sehemu yenye mkesha wa mziki, au kiwandani
 đź‘‰maumivu ya mwili au kidonda
 đź‘‰magonjwa ya akili mfano SCHIZOPHREMA /DOMENTIA
 _MADHARA YA KUTOKUPATA USINGIZI VIZURI (ISOMNIA)
 madhara ya kutokulala vizuri ni makubwa sana kwani hushusha Kinga ya mwili na kuleta magonjwa makubwa Zaidi eg usahaulifu, kutokuweza kaamua mambo mazito, pia huharbu mfumo wa akili na ubongo na pia huchangia ongezeko la magonjwa yafuatayo :
 1)KUONGEZEKA KWA TATIZO LA UKOSEFU WA KUPATA CHOO (COSTIPATION)
 tatizo hili huchangiwa na ukosefu wa usingizi na huweza kuleta madhara makubwa Zaidi na kusababisha KIFO
 2)UGONJWA WA MOYO
 Mtu anapokosa usingizi mfumo wa uzalishaji homoni huvurugika ambapo uzalishaji wa homoni za stress (stress homoni) huongezeka na kusababisha vidonda vya tumbo hivyo huleta Hali ya kuhisi njaa kwa muda mfupi baada ya kutoka kula na katika Hali hii humfanya kuwa na HASIRA na ghadhabu
 3)SHINIKIZO LA DAMU
 ukosefu wa usingizi huchangia ongezeko la shinikizo la damu kwa asilmia kubwa pia huchangia kuzeeka haraka kutokana na kuvurugika kwa uzalishaji homoni za ongezeko la umri, hii hufanya mtu kuonekana mzee au mtu mzima ilhali ana umri mdogo na pia humfanya mtu kuwa na HASIRA za haraka haraka
 MATIBABU NA JINSI YA KUJIKINGA NA TATIZO HILI
 matibabu ya ugonjwa huu yamegawanyika katika sehemu mbili ambazo ni MATIBABU YASIYOTUMIA DAWA NA MATIBABU YANAYOTUMIA DAWA (NON PHARMACOLOGICAL TREATMENT/PHARMACOLOGICAL TREATMENT) kama unasumbuliwa na tatizo hili jua kwamba sio wewe peke yako unasumbuliwa na tatizo hili hivyo usiogope na kujipa mawazo,kiasili kichocheo cha kuleta usingizi MZURI mwilini hujulikana kama MELATONIN
 MELATONIN hii ni homoni inayopatikana na kutengenezwa na tezi ya endocrine, tezi hii hupatikana katika ubongo wa Mnyama na binadam, pia tezi hii ndio inashikilia maisha yetu wanadamu kwa asilmia kubwa, hivyo ili kuweka mazingira Mazuri ya kupata usingizi na kuepukana na ugonjwa huu unatakiwa kufanya yafuatayo :
👉Epuka kutumia simu au laptop saa moja kabla ya Kulala
 đź‘‰epuka kulala huku taa inawaka
 đź‘‰jiwekee ratiba ya kulala na hakikisha hauvunji ratiba hiyo kila siku
 đź‘‰pendelea KUNYWA asali mbichi kabla ya kulala hii husaidia kuleta usingizi MZURI
 đź‘‰usilale karibu na vifaa vya umeme na sumaku
 đź‘‰kunywa maziwa ya yoghurt kabla ya kulala

 KAMA UNASUMBULIWA NA TATIZO HILI USISITE KUNITAFUTA 0689538628 TUTAKUPATIA DAWA YA MELATONIN AMBAYO INASAIDIA KUREKEBISHA NA KUPONYESHA TATIZO HILI LA ISOMNIA