BREAKING
BannerFans.com

Alhamisi, 17 Novemba 2016

SABABU ZA MWANAMKE KUKOSA HEDHI KWA WAKATI

FAHAMU SABABU ZA MWANAMKE KUKOSA HEDHI /KUTOPATA HEDHI KATIKA MPANGILIO MAALUMU (AMENORRHEA)

Asaalam alaykum warhmatullah wabarakatul ndugu msomaji wa page hii, napenda kukushukuru kwa kuungana Nami katika page hii kuendelea kutoa elimu kwa wanawake na wasichana kuepukana na magonjwa mbalimbali yanayosababisha kukosa hedhi iliyo salama, kutokana na maswali yenu ya kwanini mwanamke huwa anakosa hedhi ilhali Hana mimba??nimeona ni vyema kuelezea hili tatizo kwa undani ili muweze kutambua vizuri tatizo hili ambalo kitaalamu linajulikana kama AMENORRHOEA

AMENORRHEA NI NINI??
hii ni hali ya mwanamke ambaye amepevuka na kukomaa maumbile yake ya Uzaz kushindwa kupata hedhi/kupitiliza siku za hedhi
~kwa ufupi tatizo hili limekua likiwakumba na kuwaletea usumbufu wa kisaikolojia wanawake wengi wakidhani kwamba wamepata ujauzito nk, hata hivyo tatizo hili la kukosa hedhi linaweza kutokea awali au baadae kabisa maishani
~kuna aina mbili za tatizo hili (amenorrhea)

(1)PRIMARY AMENORRHEA ~hii ni hali ya kukosa hedhi inayomtokea mwanamke/msichana aliye katika umri wa kuvunja ungo ambapo Hali hii huweza kuendana na kutopata mabadiliko ya kimaumbile yanayoambatana na kuvunja ungo kama vile KUOTA NYWELE SEHEMU ZA SIRI, KUOTA MATITI, NK ila bado hapati siku zake

(2)SECONDARY AMENORRHEA ~hii ni hali ya kukosa hedhi inayomtokea mwanamke ambaye si mjamzito wala hanyonyeshi na ambaye hajakoma hedhi na wala hatumii dawa za Uzazi wa mpango ambapo awali alikua akipata hedhi kama kawaida Lakini akasimama kwa muda huenda ni miezi au mwaka mzima hapati hedhi mpaka sasa

~NAMNA AMBAVYO MWANAMKE HUPATA HEDHI
Kwa Kawaida ili mwanamke apate hedhi katika mzunguko ulio Sawa ni lazima tezi ya hypothalamus na pituitar pamoja na kiwanda cha mayai(ovaries) viwe vinafanya kazi kwa ushirkiano yani sawasawa

~VYANZO VYA TATIZO HILI
Vyanzo vya tatizo hili vyaweza kuwekwa katika Makundi makuu matatu ambayo ni vile vinavyohusisha matatizo katika mfumo wa homoni, vile vinavyohusisha matatizo katika tezi ya pituitar, mfumo wa Uzazi na vile vinavyohusisha mabadiliko katika mwili wa mwanamke visababishi hivyo ni ÷
👉matatizo katika hypothalamus ambapo matatizo haya husababisha ÷uvimbe katika ubongo karibu na tezi ya pituitar, ukosefu au upungufu wa homoni zinazochochea kukua na kufanya kazi kwa via vya Uzazi,

👉uzito mdogo kuliko Kawaida

👉pituitar kushindwa kufanya Kaz vzur baada ya seli zake kufa hii ni iwapo mama alipoteza damu nyingi wakati wa kujifungua

👉kuwepo kwa kiwango kikubwa cha homoni ya prolactin katika damu (PROLACTINEMIA)
(proclatin ni homoni inayochochea uzalishaji wa maziwa wakati wa kunyonyesha hivyo Hali ya kuwa proclatin nyingi katika damu husababisha kukosa hedhi

👉kuwa na msongo wa mawazo ni hatari

👉kuziba kwa utando unaozunguka uke (HYMEN) hivyo kukosekana tundu la kupitishia damu (IMPERFORATE HYMEN)

👉 Mazoezi makali ya mwili na ulaji mdogo wa Chakula, tabia hii hushusha homoni ambayo inahusika na kuweka siku zako katika Hali nzuri yani hufanya leptin kuwa katika kiwango cha chini sana hivyo ni hatari

👉ugonjwa wa kurithi wa GALACTOSEMIA unaoambatana na kuwa na kiwango kidogo cha sukari aina ya GALACTOSE katika damu

👉baadhi ya magonjwa ya viungo vya Uzazi yamekua yakiambatana na kusimama kwa hedhi mfano wa magonjwa hayo ni POLYCYSTIC OVARIAN SYNDROME

👉MENO PAUSE ~hii ni hali ambayo hutokea kipindi cha miaka 42_55 homoni zinazohusika na kupata hedhi huwa Kwenye kiwango cha chini sana kiasi hufanya haziwezi kufanya Kazi sawasawa

DALILI ZA TATIZO HILI
👉Mwanamke kuwa na vinyweleo vingi na kuota ndevu hii inamaanisha na kuashiria kuwepo kwa kiwango kikubwa cha homoni za kiume za ANDROGEN

👉kuongezeka uzito kupita kiasi

👉matiti kutoa maziwa wakati mwanamke si mjamzito wala hanyonyeshi

👉mwanamke kuwa na mhemko kuliko Kawaida

👉 uke kuwa mkavu

👉kutokwa jasho sana wakati  wa usiku

👉mabadiliko katika kupata usingizi vinaweza kuashiria kuwepo kwa tatizo katika ovaries

👉kutokupata hedhi katika mpangilio

MATIBABU
NA JINSI YA KUJIKINGA NA TATIZO HILI
matibabu ya kukosa hedhi yanaweza kutibiwa hospital kutokana na chanzo cha tatizo ambapo huwa ni kupewa dawa au kufanyiwa upasuaji pale patapobidi

NOTE :Ni vizuri kuongea na daktari ili ajue ni kwa namna gan atakusaidia pia waweza kufanya mambo yafuatayo ili kujiepusha na tatizo hili

👉ZINGATIA ULAJI ULIOSAHIHI AMBAO UNAHUSISHA ULAJI WA MATUNDA KWA WINGI NA MBOGA ZA MAJANI

👉TUMIA MAZIWA YA SOY /JUICE YA WATERMELON/MAJI YA MSHUBIRI

👉FANYA MASAJI KWENYE TUMBO LA CHINI KWA KUTUMIA MAJI YA UVUGUVUGU (UKIWA KTK BREED) HII ITASAIDIA KUONGEZA DAMU NYINGI KUTOKA

👉KULA CHAKULA  KISICHOTOKANA NA DAMU (VEGETARIAN DIET) CHENYE PROTIN NYINGI MFANO, NAZI, MAHARAGE, KOROSHO NA KARANGA
Hakikisha unazingatia haya ili kuepukana na madhara ya huu ugonjwa ambayo ni makubwa sana

MADHARA YANAYOWEZA KUTOKEA IWAPO TATIZO HILI HALITAPATIWA MATIBABU
👉Mwanamke kuchelewa kuingia menopause hali huu ni mbaya kwani husababisha SARATAN YA MATITI kwa kias kikubwa
👉mwanamke kupata maumivu wakati wa tendo la ndoa kwasababu ya kupungua kwa hamu ya kufanya mapenzi na uke kuwa mkavu
👉husababisha matatzo ya kutopata usingizi
👉matiti husinyaa na kupata hedhi Bila mpangilio,

ndugu Rafiki msomaji Asante kwa kuwa Nami muda wote kutoa elimu hii kwa jamii kama una MAONI/ USHAUR NIANDIKIE UJUMBE KUPITIA NAMBA NA EMAIL YANGU HAPO CHINI

KUSOMA ZAIDI MAKALA ZA AFYA TEMBELEA BLOG HII
naythamhealthcare.blogspot.com

Makala hii imeandaliwa na Dr Naytham S Masoud
email-nsalum998@gmail.com
+255623026602/+255746465095

PLEASE USISAHAU KUSHARE, KUKOMENT, KULIKE NA KUWAALIKA WENZAKO KATIKA PAGE HII NI VIZURI ZAIDI UKISHARE NA WENZAKO WAPATE ELIMU HII

Hakuna maoni :