BREAKING
BannerFans.com

Jumatatu, 29 Juni 2015

VIJUE VYAKULA VINAVYOPELEKEA KISUKARI MWILINI

Ndugu karibu sana katika makala zangu ambazo huzungumzia chanzo cha tatizo, namna ya kuepuka na kutibu kabisa hilo tatizo bila kukaa kuhangaikia kutibu dalili ya ugonjwa. Ni dhahili kuwa maisha yetu ya kifahari tumekuwa tunakula vyakula vyakutosha lakini vyakula hivi si vyakujenga mwili bali vinakuja na magonjwa mengi ndani yake. Siwezi kuilaumu jamii kwa kuendelea kula vyakula hivi bila kuwa na kiasi bali ni mfumo wa afya kwa ujumla ambayo inaweka juhudi kubwa kubaini magonjwa na kutibu dalili na siyo kuweka jitihada kubwa katika kutoa elimu ya namna ya kujikinga na magonjwa na kushughurika na chanzo au mzizi wa ugonjwa. Hivyo ni jukumu letu kuhakikisha jamii inaepukana na magonjwa haya kwani tukifanya hivyo utamaduni huu wa kutuletea vyakula vinavyo dhoofisha miili yetu na hatimaye wanaleta misaada ya matibabu inayo lenga kubaini magonjwa na sio kutoa elimu ya kuzia na kupambana na vyanzo hasa vya tatizo.
Baada ya kusema hivyo basi ningependa kwa siku ya leo nizungumzie kidogo madhara ya vyakula vyenye sukari nyingi na nguvu za kiume ambazo hadi sasa wanaume ambao hawawezi kutungisha mimba idadi inaongezeka. Kumekuwa na usemi kuwa upungufu wa nguvu za kiume unahusishwa sana na kuzeeka kwa mtu. Ni dhahiri kuwa kuzeeka kwako sio chanzo cha wewe kupata upungufu wa nguvu za kiume na hutakiwi kuhusisha bali ni tabia yako inayo ambatana na ulaji wa vyakula na unywaji wa vinywaji vyenye sukari nyingi,unywaji pombe,uvutaji sigara, utumiaji wa madawa ya hospitali bila ushauri maalumu na pia utumiaji madawa ya hospitali pale unapotibu ugonjwa flani kwa mfano dawa za kifafa, dawa za usingizi na dawa za dege dege,utumiaji wa madawa ya kulevya na kujichua kila siku. Hivyo maisha yetu ya kila siku ndio chanzo cha ukosefu wa nguvu za kiume
NINI MCHANGO WA VINYWAJI VYENYE SUKARI NYINGI NA VYAKULA VYA VIWANDANI KATIKA UPUNGUFU WA NGUVU ZAKIUME
Tumekuwa tukiishi mazingira ya kula vyakula vya sukari kila siku kwa mfano, ukiamka asubuhi unakula mikate, tafiti zinasema kuwa mkate una aina ya wanga iitwayo amylopectin A ambayo endapo ikimeng”enywa ni chanzo cha sukari nyingi sana kwenye damu. Pia unatakiwa kufahamu kuwa slice mbili za mikate ni sawa kama umeramba vijiko viwili vya sukari ya mezani yani sukari nyeupe. Hivyo mikate ni moja ya vyakula vyakuepuka sana kama unahitaji kuwa na afya njema na mwenye nguvu za kiume tele. Pia imekuwa ni kawaida unaamka asubuhi na soda kwani hii ni ishara kuwa tayari kiini mahususi kwenye soda ambacho huitwa ASPARTAME kimesha kuaathiri na umekuwa addicted na vyakula vya sukari. Aspartame ni kiambata mahususi kwenye vinywaji vya coka na hivyo kimewekwa humo ili kukufanya uwe na hamu ya kunywa soda mara kwa mara au kula vyakula vitamu vitamu. Kiini hiki huenda kwenye ubongo na kujishika kwenye vipokea taarifa yani receptors na kutoa taarifa ambazo zina angamiza mwili wako.
Sukari inapozidi mwilini inasababisha uchovyaji wa insulin kwa wingi ambayo hupunguza kiasi cha testosterone ndani ya ndamu na hatimaye kupunguza nguvu na shauku ya tendo la ndoa. Kulingana na utafiti uliofanywa kwa kutumia kipimo cha sukari kiitwacho ORAL GLUCOSE TORELANCE TEST AU OGT kilionesha kuwa wanaume wenye sukari nyingi kwenye mzunguko wa damu walionesha kiwango kidogo cha kichocheo cha nguvu za kiume kiitwacho testosterone ambacho hushughurika na sifa za kiume,kutengeneza mbegu za kiume na kuimarisha misuli bila kusahau nguvu za kiume. Ni dhahili kuwa ongezeko kubwa la wanaume ambao wana matatizo ya nguvu za kiume inasababishwa na ulaji na unywaji wa vyakula vyenye sukari nyingi. Hivyo basi ni dhahiri kuwa kama una tatizo hilo linaweza kukupelekea kukosa mototo kwani hata manii ya kiume kutengenezwa kwake itakuwa ni kwa shida sana. Epuka hivi vyakula na jua namna gani unaweza rudisha afya yako mwanzo kwa kutumia vyakula na virutubisho mahususi vinavyo ondoa tatizo la nguvu za kiume.
Pia vyakula vya sukari nyingi hupunguza kwa hali ya juu vichocheo vya kujenga mwili yani GROWTH HORMONE ambayo hutolewa na tezi ya pituitary wakati wa usingizi mzito. Kichocheo hiki cha kujenga mwili yani GROWTH HORMONE kinafanya kazi kubwa ya kutumia mafuta yaliyohifadhiwa kwa matumizi ya ziada, pia growth hormone huimarisha misuli ya mwili na kuimarisha nguvu za kiume. Hivyo kupungua kwa kichocheo hiki husababisha mrundikano wa mafuta mabaya na kutengeneza nyama zembe yani BELLY FAT, kuongezeka uzito,kupata kizuizi cha insulin na hatimaye kisukari aina ya pili.
Vyakula vya sukari nyingi hukufanya muda wote ujihisi umechoka na huna nguvu ya kufanya kazi yoyote na wengine hufikiria kuwa wanasumbuliwa na ugonjwa wa malaria. Hii ni kwa sababu sukari nyingi kupita kiasi inasababisha utoaji wa insulin kuongezek a ili kupunguza sukari hiyo na matokeo yake kusababisha njaa na shauku ya kula mara kwa mara kwa sababu ya kupungua kwa reptin hormone inayotolewa na seli za kuhifadhi mafuta. Pia sukari nyingi huzuia utengenezwaji wa kichocheo kiitwacho OREXIN ambacho husafirisha taarifa na kuongoza kitendo cha ulaji na kukufanya uwe na nguvu ya kuwa macho na kufanya kazi zako. Sasa orexin inapopungua inasababisha muda wote kukaa umechoka na unasinzia ovyo ovyo. Ni dhahiri kuwa inaweza kuwa unasema hii makala ni miongoni mwa waathiriwa wa sukari nyingi kwani uzito umekuzidi,kitambi,unasinzia ovyo ovyo na muda wote umechoka. Usihofu na usikate tama chakula cha matunda na mboga mboga ndio suluhisho lako kama wewe huwezi kutumia hivi basi jitahidi kutafuta virutubisho vyenye kurudisha afya yako upya bila usumbufu kabisa.
Pia sukari nyingi kwenye damu husababisha msongo wa mawazo sana na hatimaye kusababisha utolewaji wa vichocheo vya CORTISOL ambayo husababisha ulaji ovyo wa vyakula wa bila mpangilio. Mtu kama huyu utakuta unakula pale pale baada ya muda mfupi tena njaa. Hivyo tujifunze namna gani sasa unaweza kuirudisha afya yako bila tena kuendelea kuongeza sumu mbali mbali mwilini. 
Napenda nikupongeze msomaji wangu ni jukumu lako kujua nini cha kufanya kama wewe bado ujafikia ku athiriwa na tatizo hili. Hivyo basi nina imani utailinda afya yako na kuipenda. Chakula cha mimea na matunda kinakuweka mbali na dawa hizi wapenda kwani tusipende kula vyakula vyenye nembo ya kuisha muda wake. Kwa Yule tayari ameshakubwa na tatizo hili kwa sababu ya matumizi ya sukari nyingi napenda kukuambia kuwa CHAKULA PEKEE NI TIBA KABISA NA KUJIEPUSHA NA DAWA ZA KILA SIKU UNAZO NUNUA AMBAZO HAZITIBU TATIZO. Kama huwezi kupangilia chakula chako vizuri na namna ya kurudisha tatizo lako unaweza tumia viutubisho vinavyo ondoa tatizo na kurudi kuwa kijana. Kama ukihitaji tunaweza kukuelekeza namna ya kukipata au tupigie

Hakuna maoni :