BREAKING
BannerFans.com

Jumapili, 9 Oktoba 2016

JE, WAZIJUA FAIDA ZA TANGAWIZI NA ASALI? SOMA HAPA ILI KUFAHAMU

FAHAMU FAIDA 48 ZA JUISI YA TANGAWIZI AMBAZO ULIKUWA HUZIJUWI ;
Asaalam alaykum warhmatullah wabarakatul mpenzi msomaji wa page hii, ni matumaini yangu umzima kabisa,kumradhi Kwa ukimya wangu nilibanana na majukum ya hapa na pale ila sasa namshukuru ALLAH wepesi umepatikana na nimeweza kurejea tena hapa,
Leo napenda tufaham faida za tangawizi mwilini ambazo ni ...

1. Huondoa sumu mwilini haraka sana,

2. Huua bakteria wa aina nyingi mwilini hata salmonella ndani ya mwili hata juu ya ngozi,

3. Kuna viua vijasumu (antibiotics) vya asili viwili kwenye tangawizi,

4. Huondoa uvimbe mwilini,

5. Huondoa msongamano mapafuni,

6. Tangawizi inayo ‘zingibain’ ambayo huua vimelea mbalimbali vya magonjwa na mayai yake,

7. Huondoa maumivu ya koo,

8. Huua virusi wa homa,

9. Huondoa maumivu mbalimbali mwilini,

10. Huondoa homa hata homa ya baridi (chills),

11. Hutibu saratani ya tezi dume. Tangawizi huua kimeng’enya ambacho ni chakula cha seli za kansa ya tezi dume kiitwacho ‘5-LO enzymes’ na seli hizo za kansa hufa ndani ya masaa mawili au manne bila hicho kimeng’enya.

12. Tangawizi ina kiinilishe mhimu sana ambacho huzuia kuongezeka kwa seli za kansa ya kongosho kiitwacho kwa kitaalamu kama ‘gingerol”

13. Hutibu kansa zinazoweza kusababishwa na kupata choo kigumu muda mrefu (constipation-r
elated cancer)

14. Ni dawa nzuri kwa kansa ya kwenye damu (leukemia)

15. Ni dawa nzuri dhidi ya kansa ya mapafu (lung cancer)

16. Huzuia kujizalisha kwa bakteria aitwaye ‘Helicobacter pylori’, bakteria huyu ndiye husababisha vidonda vya tumbo mwilini, pia hutibu kiungulia, na kanza mbalimbali za tumbo,

17. Ni msaada sana katika kuzuia na kutibu kansa ya titi,

18. Hutibu kanza za kwenye kizazi na kanza za kwenye mirija ya uzazi,

19. Huongeza msukumo wa damu,

20. Husaidia kuzuia shambulio la moyo,

21. Huzuia damu kuganda,

22. Hushusha kolesto,

23. Husafisha damu,

24. Husaidia watu wenye kukakamaa kwa mishipa,

25. Hutibu shinikizo la juu la damu,

26. Husafisha utumbo mpana,

27. Hupunguza mishtuko kwenye utumbo mpana na tumbo kuunguruma,

28. Huondoa GESI TUMBONI KIRAHISI ZAIDI,

29. Husaidia mfumo wa mmeng’enyo wa chakula,

30. Dawa nzuri ya kuondoa uchovu,

31. Husaidia kuzuia kutapika. Husaidia hata wale wanaosafiri baharini wasipatwe na kichefuchefu,

32. Husaidia kuondoa maumivu kutokana na mkao mmoja wa mrefu ama kusimama au kukaa,

33. Husaidia uzalishwaji wa juisi vimeng’enya kwa ajili ya kumeng’enya chakula,

34. Husaidia kuzuia kuharisha,

35. Husaidia mfumo wa upumuaji na kutuliza dalili za pumu,

36. Hutibu tatizo la miguu kuwaka moto
37. Hutibu homa ya kichwa,

38. Hutibu maumivu ya tumbo wakati wa hedhi,

39. Hutibu homa za asubuhi hata kwa mama mjamzito,

40. Husaidia kupunguza homa ya baridi yabisi (helps reduce inflammation of arthritis),

41. Huimarisha afya ya figo,

42. Husaidia kupunguza uchovu unaotokana na matibabu yaliyopita ya mionzi
43. Ina madini ya potassium ya kutosha,

44. Ina madini ya manganese ambayo ni mhimu katika kuuongeza mfumo wa kinga ya mwili dhidi ya magonjwa mbalimbali, hulinda kuta za moyo, hulinda mishipa ya damu na mishipa ambako mikojo hupita,

45. Ina kitu kinaitwa ‘silicon’ ambacho chenyewe kazi yake hasa ni kuongeza afya ya ngozi, nywele, meno na kucha,

46. Husaidia umeng’enywaji wa madini ya calcium,

47. Pia ina vitamini A, C, E, B-complex, chuma, zinki , magnesium, phosphorus, sodium, calcium, na beta-carotene,

48. Hulinda kuta za moyo, hulinda mishipa ya damu na mishipa ambako mkojo hupita

Asante Kwa kuwa nami rafiki naomba usikose kushare na wengine ili waweze kutambua faida hizi pia kama unasumbuliwa na tatizo lolote lihusuyo afya usikose kuwasiliana nami ili kuweza kupata Ushauri zaidi

PIA KUSOMA MAKALA MBALIMBALI ZA AFYA USIKOSE KUTEMBELEA BLOG HII
naythamhealthcare.blogspot.com

 Makala hii imeandikwa na Dr Naytham S Masoud
Email -nsalum998@gmail.com
+255623026602/+255746465095

TAFADHALI SHARE NA WENGINE UJUMBE HUU WAPATE KUJIFUNZA

Hakuna maoni :